Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba (kushoto)
akibadilishana mawazo na Balozi wa Sweden Nchini, Katarina Rangnitt
(kulia) katika kikao chake kilichofanyika katika Ofisi ya Makamu wa Rais
jijini Dar es Salaam tarehe 12 Oktoba, 2017. Kikao hicho
kilishirikisha pia wataalamu kutoka Idara ya Mazingira. Katikati ni
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora.
Balozi wa Sweden Nchini Bi.
Katarina Rangnitt (wa pili kulia) akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba mara baada ya
kumtembelea hii leo Ofisini kwake Mtaa wa Luthuli Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine Mhe. Balozi amezungumzia namna ya kushirikiana
katika sekta ya Mazingira.
Balozi wa Sweden Nchini Bi.
Katarina Rangnitt na Naibu Balozi wake Bw. Ulf Kallstig ambae pia ni
Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wakiwa Ofisini kwa Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January
Makamba mara baada ya kufanya mazungumzo hii leo.