![]() |
| Kocha Msaidizi wa Mbeya city Ndugu Maka Mwalwisi akizungumza na Blog hii juu ya tetesi za yeye kuachana na Mbeya Mbeya Msimu huu |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Zikiwa zimebaki siku chache kuanza kwa msimu Mpya wa Ligi kuu Vodacom
Tanzania Bara Timu ya Mbeya City Fc
inayoshiriki Ligi hiyo huenda wakanza vibaya kutokana na kuondokewa na Kocha
Msaidizi wa Timu hiyo .
Taaria za kuondoka kwa Kocha zilianza kuenea katika maeneo
mbalimbali katika jiji la Mbeya hali ambayo iliiradhimu blog hii kumtafuta kocha huyo ili kuweka bayana juu ya
yeye kuondokana na Timu hiyo.
Akizungumzia sakata hilo Kocha huyo Msaidizi wa Mbeya City Maka
Mwalwisi,amesema kitendo cha yeye kuendelea kukinoa kikosi hicho ni kujifungia
uwezo na ujuzi wake wa kufundisha hivyo wakati umefika wa kutafuta
timu nyingine na kuiendeleza.
Aidha amebainisha wazi kuwa mkataba wake ndani ya Mbeya City ulimalizika
Mei 30 mwaka huu ambapo katika kipindi hicho alifanikiwa kupata nafasi ya
kwenda kupata mafunzo ya wiki mbili yaliyoandaliwa na CAF na kufanikiwa kupata
lesseni daraja B.
Amesema, mafunzo hayo ambayo makubwa nchini Tanzania
kwa makocha yamechangia yeye kufanya maamuzi ya kupima uwezo wake kwa kutafuta
timu ambayo ataanza nayo kuanzia ligi daraja la kwanza mpaka hapo itakapofikia.
Amesema, kila kocha anapoishika timu na kuifundisha hutumia ujunzi
na uwezo wake hivyo kitendo cha yeye kuendelea kubaki Mbeya City ni kufungia
ujuzi wake kabatini.
Aidha, Kocha Maka amewaomba mashabiki kuendelea kuipa ushirikiano
timu ya Mbeya City kwani anaamini ya kwamba timu hiyo ikiwa na kikosi chake
kile kile itaendelea kufanya vizuri ndani na nje ya nchi.
Aidha Maka amesema kuwa changamoto anayoiona mbele ya timu hiyo ni
hatua ya wachezaji kuwa mbali nay eye kwani amekuwa na wachezaji kwa muda mrefu
kabla ya hata kujiunga na mbeya city.
Amesema kuwa kikubwa ambacho wachezaji hao watakikumbuka kwa kocha
huyo ni hatua ya kuwaweka karibu na kuondoa tofauti zao pamoja na kuwaanda
vyema kukabiliana na changamoto za kimchezo na maisha ya kimpira kwa ujumla
wake.
Hata hivyo, hakusita kummwagia sifa kocha Juma Mwambusi ya kwamba
ni mwalimu mzuri huku akiupongeza uongozi wa timu nzima ya Mbeya City kwa kuwa
na utaratibu mzuri wa uendeshaji wa timu kwani mpaka sasa anachokifahamu ni
kwamba timu hiyo haijatoa mchezaji nje bali inatarajia kuingiza wachezaji.
Wakati huo amewataka wapenzi
wa Timu hiyo ya Mbeya City pamoja na wadau kwa ujumla kutoa weka fikra zozote
mbaya juu ya yeye kuondoka mbeya city badala yake waione kama sehemu tu
changamoto katika harakati za kimchezo
Mwisho.







Post a Comment