Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kamanda wa Polisi Mkoani mbeya Ahmed Msangi


EmanuelMadafa,MBEYA
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya limewahakikishia wananchi wa mkoa  kusherekea sikuku ya pasaka kwa amani na Utulivu.

Aidha, Jeshi hilo linatoa wito kwa Kila Mwananchi kuona wajibu  wa kufuata na kutii sheria zilizowekwa bila kushurutishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Mbeya Kamanda wa Polisi Mkoani humo Ahmed Msangi amesema katika kuelekea katika sherehe za sikuku Pasaka jeshi hilo limejipanga vyema katika kuhakikisha wananchi wa mkoa wa mbeya wanasherekea kwa amani na Utulivu.

Hata Hivyo Kamanda Msangi amewataka wazazi na walezi mkoani humo  kuacha muangalizi/waangalizi nyumbani wanapotoka kwenda katika Ibada za Mkesha na Sherehe kwa jumla kwa ajili ya ulinzi na usalama wa mali zao.

Pia amewataka  watumiaji wa Vyombo vya Moto kuhakikisha wanafuata na kuzingatia Sheria na Alama za Usalama Barabarani ili kuepuka ajali Pamoja na watembea kwa miguu kuwa makini na matumizi ya barabara ikiwa ni pamoja na kuvuka katika maeneo yenye vivuko [zebra crossing].

Aidha Kamanda wa Polisi anawataka wazazi/walezi kuwa makini na watoto wadogo kwa kutowaacha wakatembea bila uangalizi wa kutosha.

Pamoja hali hiyo pia Wamiliki wa kumbi za Starehe kuhakikisha  wanazingatia taratibu za uendeshaji wa Biashara zao ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza.
Mwisho


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top