Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Abbas Kandoro akitia saini kitabu cha maombolezo.

Kandoro akiwafaliji wafiwa


Spika Anne Makinda akiteta jambo na Waziri Hawa Ghasia ambapo katika mazishi hayo waziri ghasia amemuwakilisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Picha stori kwa hisani ya Francis Godwin Blog


Na Mwandishi wetu,Iringa

WAZIRI wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa Ghasia leo  amemwakilisha  waziri  mkuu Mizengo Pinda katika mazishi  ya  aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Marehemu Moshi Chang'a.

Katika mazishi  hayo yalihudhuriwa na mamia  ya  wakazi  wa Manispaa ya  Iringa na viongozi  wa serikali  kutoka mikoa mikoa  mbali mbali nchini pia  spika  wa  bunge Anne Makinda  alitumia nafasi hiyo  kuueleza  umma siri  nzito  iliyofichika  dhidi yake ya marehemu Chang'a mwaka 1995 wakati wa uchaguzi mkuu wa kwanza  ulioshirikisha vyama  vingi kuwa bila marehemu huyo asingeweza kuwa mbunge kutokana na kubanwa na chama cha upinzani cha NCCR Mageuzi kwa  kipindi  hicho

Akizungumza   wakati wa kutoa  salama  mbali mbali kwa  viongozi  mjini  Iringa Spika Makinda  amesema  kuwa kwa mara ya kwanza  mwaka 1995  alibanwa kupita  kiasi na  NCCR Mageuzi  katika jimbo lake la uchaguzi la Njombe kusini na  kuwa  bila marehemu  huyo ambae kwa kipindi  hicho alikuwa ni katibu wa CCM wilaya ya Njombe kamwe asingeweza kuwa mbunge .

Kwa  upande  wake  mkuu wa  mkoa wa Mbeya  Abas Kandoro  akimuelezea  Chang'a wakati wa kutoa  salam  hizo  amesema  kuwa  kamwe  hata  sahau utendaji kazi wa mkuu  huyo wa wilaya  ambae amepata  kufanya nae kazi katika wilaya ya Makete ambapo  yeye akiwa mkurugenzi Chang'a alikuwa ni kiongozi wa  CCM wilaya  hiyo  na baada ya kwenda Mbeya  pia  Chang'a amefanya kazi kama mkuu wa wilaya katika mkoa  huo  .

Kandoro amesema kuwa  utendaji  kazi na utumishi  uliotukuka wa  Chang'a ni mfano  wa  kuigwa kwa watumishi wengine wa umma katika Taifa  hili.

Aidha Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dr Christine Ishengoma  amesema kuwa mkoa  wa Iringa  umepata  pigo kubwa kwa  kifo cha mkuu  huyo wa wilaya  hasa ukizingatia mchango mkubwa wa kimaendeleo ambao amepata  kuonyesha ndani ya mkoa na nje ya mkoa na kuwa kamwe  mkoa  utaenzi yote aliyoyaacha .

 Mkuu wa  mkoa  wa Rukwa injinia Stella Manyanya  amesema kuwa  mkoa  wake amempoteza  kiongozi mzalendo na aliyependa kazi yake na kuwa hata  akiwa  safarini hakuwa na shaka na utendaji kazi wa mkuu  huyo wa  wilaya na kuwa  siku  zote mbali ya kuongoza kama kiongozi wa serikali ila wakati mwingi alitumia  kuwahubiria upendo  wananchi wa  wilaya  yake.

Kwani  alisema kuwa alikuwa hawezi kuanza mkutano  bila kumhubiri  mwenyezi Mungu mbali ya kuwa  yeye alikuwa muumini wa dini ya Kiislam ila alikuwa akihubiria dini ya kikristo  .

Hata  hivyo  amesema kuwa  hadi  kesho anaamini  alishinda  ubunge  jimbo hilo mwaka 1995 si kwa uwezo wake  bali  alishinda kwa uwezo wa marehemu Chang'a ambao  alionyesha  uwezo mkubwa  wa kumnadi na hata kufanikiwa  kuwa mbunge wa  jimbo hilo na leo  kuwa  spika wa bunge .

Viongozi  wengine  waliopata  kushiriki katika mazishi hayo ni pamoja na viongozi  msaidizi wa Rais Jakaya Kikwete katika masuala ya siasa Ikulu Rajab Luhwavi pia viongozi kutoka mkoa wa Mwanza , Singida ,wabunge  wa bunge la jamhuri ya muungano  akiwemo mbunge wa  viti maalum mkoa  wa Iringa Ritta Kabati na Lediana Mafulu (CCM) naibu  waziri wa maliasili na utalii Mahamudu Mgimwa ambae  pia ni mbunge wa  jimbo la Mufindi kaskazin,baadhi ya  wajumbe wa bunge la katiba  kutoka mkoa  wa Iringa na wakuu wa wilaya mbali mbali akiwemo mkuu wa wilaya ya Kibondo Venance Mwamwoto mkuu wa  wilaya ya Iringa Dr Letisia Warioba ,mkuu wa wilaya ya Kilolo Gerald Guninita  na wengine  wengi 

mwisho

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top