Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Mmoja wa wajumbe akichangia maada katika kikao hicho


Na EmanuelMadafa,Mbeya

WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais, anayeshughulikia utawala bora, George Mkuchika, amesema  vitendo vya watendaji wa halmashauri kujiuhusisha na wizi wa fedha za miradi ya maendeleo   kumetokana na Madiwani kushindwa kutambua majukumu yao.

Waziri Mkuchika am,esema hayo jijini Mbeya wakati akizungumzia suala la utawala bora na rushwa jinsi zinavyoathiri utekelezaji wa miradi ya maendeleo, katika kikao cha kamati ya ushari ya Mkoa (Rcc) Mbeya.

Amesema, Madiwani wamekuwa  hawatambui wajibu wao katika kusimamia fedha zote za miradi ya maendeleo pamoja na utoaji wa tenda mbalimbali  kwenye halmashauri zao hivyo kutoa mianya ya rushwa kwa watendaji.

Amesema, endapo  vitendo hivyo havitasimamiwa au kudhibitiwa , Taifa halitaweza kuwa na maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi.

Akizungumzia suala la vitendo vya rushwa , amesema katika matukio 288 yaliyolipotiwa katika Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa  nchini (Takukuru)  kwa mkoa wa Mbeya, halmashauri ndizo ziliongoza kwa kuwa na jumla ya tuhuma 65.

Amezitaja sekta nyingine kuwa ni Mahakama kuwa tuhuma (46), polisi (35), sekta binafsi (35), huku serikali Kuu, uhamiaji, Maliasili, Taasisi za dini, Jeshi la wananchi (JWTZ) na vyombo vya habari zikiwa na jumla ya tuhuma moja tu kila mojawapo.

Aidha, Mkuchika amezitaka halmashauri zote nchini  kuandaa utaratibu wa kuwaita na kuwashirikisha Takukuru katika vikao vyao vya kujadili masuala ya maendeleo  .

Akizungumzia vitendo vya Rushwa , Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Mbeya, Felix Wandwe, alisema  licha a kushughulikia rushwa ndogo ndogo TAKUKURU pia imeendelea  na uchunguzi wa kuendesha kesi za rushwa kubwa mahakamani.

Hata hivyo amebainisha kuwa  kwa Mkoa wa Mbeya kuanzia mwezi Januari hadi Desember 2013 jumla ya  matukio ya rushwa 288 yaliyolipotiwa katika taasisi hiyo huku majalada 42 yakiwa tayari yamechunguzwa na kukamilika.
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top