Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na EmanuelMadafa,Mbeya
POLISI Mkoani Mbeya inawashikiliwa raia 82 wa nchini  Ehtiopia kwa kosa la kuingia  Tanzania bila ya kibali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetoka juzi majira ya saa mbili usiku katika Kijiji cha Busale Wilayani Kyela  Mkoani Mbeya.

Amesema, uchunguzi wa awali umebaini kwamba raia hao wa kigeni waliingia nchini wakitokea nchi ya Malawi baada ya serikali ya nchi hiyo kuwafukuza..

Amesema, katika harakati za kukimbilia nchini Tanzania raia wema waliwaona na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi zilizofanikisha kuwatia nguvuni watu hao.

Amesema, taratibu zinafanywa ili watuhumiwa kukabidhiwa kwenye idara ya Uhamiaji huku akiwataka wageni wa kutoka nchi za nje kujenga tabia ya kufuata taratibu za kisheria pindi wanapotaka kusafiri kwenda nchi nyingine.

Hata hivyo Kamanda Msangi, ameendelea kuwaomba wananchi kujenga tabia ya kutoa taarifa polisi mara wanawatilia watu mashaka dhidi ya vitendo vya uhalifu.
Mwisho
Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top