Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Lukas Mwampiki aliyekuwa katibu mwenezi Mbeya
Na EmanuelMadafa,Mbeya
CHAMA  cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Mbeya kimemvua nyadhifa zote Katibu Mwenezi wa Wilaya ya Mbeya mjini Lukas Mwampiki ambae ni Diwani wa Kata ya Mwakibete.

Akizungumza na Blog hii Mwenyekiti wa Chadema Wilaya, John Mwambigija amesemakwamba  Mwampiki na mwenzie Jocob Kaluwa ambaye ni mjumbe wa kamati tendaji ya Wilaya wamebainika kukihujumu chama  kwa kuvujisha siri za chama nje.

Nyadhifa alizovuliwa  Diwani huyo ni Ukatibu Mwenezi wa Wilaya na nafasi ya Uwenyekiti wa Ulinzi na Usalma Kanda za  Nyanda za Juu Kusini huku Kaluwa akiondolewa nafasi yake ya ujumbe wa kamati tendaji.

Mwampiki na mwenzie licha ya kuvuliwa nyadhifa hizo pia wamesimamishwa kutoshughulika na kazi za chama mpaka uchunguzi utakapokamilika na kwamba endapo watabainika kuhusika na tuhuma hizo hatua za kinidhamu zitachukuliwa ikiwa na kuvuliwa uanachama.

Mwambigija, amesema Katibu Mwenezi huyo ametajwa kuhusika na usambazaji wa nyaraka za ofisi nje kwa viongozi wa Kata kinyume cha utaratibu. 

Amesema, kitendo hicho ni utomvu wa nidhamu  hivyo chama kimewavumilia lakini kimefika mahala sasa ni vema kikawachukulia hatua za kinidhamu wahusika ikiwa na kuvuliwa uanachama endapo  tuhuma wanazokabiliwa nazo zitathibitika kuwa ni za kweli.

Akizungumzia sakata hilo la kuvuliwa  uongozi Diwani Mwampiki, amesema kwa upande wake hawezi kuzungumzia chochote kwani tayari yeye binafsi alishaandika barua ya kujihudhuru kutokana na kuchoshwa na majungu na fitina zilizopondani ya chama hicho.

Amesema, katika barua hiyo alieleza jinsi alivyochoshwa na kukerwa na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wenzake ambao wamekuwa wakiendekeza majungu, fitina na chuki zisizokuwa na sababu yoyote ya msingi zaidi ni tamaa na uchu wa madaraka.

Hata hivyo akizungumzia sakata  la kujiudhuru nafasi yake ya  ujumbe wa kamati  tendaji ndani ya chama,Kaluwa amesema  yeye ameamua kujipunguzia madaraka aliyokuwa nao ndani a chama na kutoa nafasi kwa vijana wengine kushika nafasi hizo.
Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top