Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This





Mwamuzi wa Mshindano hayo Ndugu Oscar Firbet akiapa mbele ya mgeni rasmi 

Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Mbeya Ndugu Costantine Mushi Akizindua Mashindano kwa ishara ya kupiga langoni.

 Na EmanuelMadafa,mbeya
Serikali  Mkoani  Mbeya, imewataka  waandaji wa mashindano ya Umiseta na Umitashumta  kutumia utaratibu wa  kikanda  kwenye mashindano hayo ngazi ya kitaifa ifikapo mwaka 2015.

Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Mbeya Ndugu Juma Mwaigambe,ametoa kauli hiyo leo wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Umiseta Ngazi ya Mkoa katika viwanja vya shule ya Ufundi Iyunga.

Amesema Mchakato uliopo kwa sasa ni kuanda timu ya pamoja kwa kushirikisha Halimashauri 10 za mkoa  ambazo zitapambana na Mikoa ya Rukwa na Katavi na kupata kikosi ambacho kitashiriki fainali hizo.

Amesema hatua hiyo inainyima  fursa Mkoa wa Mbeya kushiriki michuano hiyo hasa kutokana na Mkoa huo kuwa na Halmashauri nyingi ambazo zinashiriki michuano tofauti na Katavi na Rukwa zenye Halmashauri chache.

Amesema mkoa wa Mbeya unahalmashauri 10 zinazoshiriki mashindano hayo tofauti na Mikoa ya Rukwa na Katavi ambayo inahalmashauri Chache hivyo nivema waandaji wa mashindano hayo ngazi ya Tifa wakaliona hilo.

Amesema Teyari Mkoa wa Ilala ,Temeke na Kinondoni zimepewa fursa hiyo ya kuwa kanda maalumu ya kimichezo hivyo umefika wakati sasa na Mkoa wa Mbeya ukapewa heshima hiyo.

Wakati huo huo Kaimu Afisa Elimu huyo amesema kuwa bado mashindano hayo yamekuwa yakikabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa fedha .
Amesema kwa kiwango kikubwa mashindano hayo yamekuwa yakiendeshwa kwa kutegemea fedha za ada za wanafunzi ambao hata hivyo upatikanaji wenye wa ada umekuwa wa kusuasua.

Aidha kwa upande wake Afisa Utamaduni Mkoa wa Mbeya Ndugu Goerge Mbigima amesema  muitiko wa mashindano hayo kwa mwaka huu umekuwa mkubwa tofauti na mwaka jana.

Mashindano hayo ya Umiseta ngazi ya Mkoa yanafanyika ngazi ya Mkoa ambapo Halmashauri 10 za Mkoa zimeweza kushiriki Mashindano kwa lengo la kupata kikosi kitakacho shiriki Mashindano ya Kanda ambapo michunao hiyo itafanyika Mkoani hapa.
  
Mwisho

Afisa Utamaduni Mkoa Mbeya George Mbigima

Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Mbeya Ndugu Jumma Mwaigambe


Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top