![]() |
| Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu
Abbas Kandoro amezitaka Halmashauri za Mkoa huo kuhakikisha zinasimamia vyema
ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato vya ndani kwa lengo la kupunguza utegemezi
kwa serikali kuu.
Mbali na kuongeza kasi ya
ukusanyaji huo pia zimetakiwa kuongeza mchango wake katika miradi ya Maendeleo inayoibuliwa na
Wananchi.
Akizungumza jijini Mbeya
Mkuu huyo wa Mkoa wa mbeya amesema kuwa kwa mwaka 2013,14lengo ni
kukusanya jumla ya shilingi
28,117,063,902 kutokana na vyanzo mbalimbali vya mapato.
Kandoro amesema Halmashauri
za Chunya ,Busokelo,Kyela,Mbeya jiji ,Mbeya na Ileje zimekusanya zaidi ya asilimia 50 hali ambayo
inaridhisha tofauti na Momba na Mbozi Rungwe ambazo zipo chini ya asilimia 50.
Kufuatia hali hiyo ,Mkuuu
huyo wa Mkoa amewataka Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia vyema jukumu
hilo la ukusanyaji wa mapato sanjali na matumizi yake.
Amesema kuwa nivema pia
viongozi hao wakazuia uwepo wa mianya ya
upotevu wa mapato kupitia mikataba ya mawakala ambao wamekuwa
wakizilazimu Halmashauri kuvunja mikataba na kuanza upya kukusanya fedha kutoka
katika vyanzo vyake hali ambayo imekuwa ikisababisha hasara kubwa kwa Halmashauri
hizo.
Wakati huo huo Kandoro amewataka wakurugenzi
wa Halmashauri hizo pamoja na wakuu wengine wa Idara mbalimbali kuhakikisha
wanapunguza safari zisizokuwa na ulazima ambazo zimekuwa zikighalimu kiasi
kukubwa cha fedha hasa kwa mazingira ya
kudai posho.
Amesema katika bajeti ya
2013 ,14 kamati za bunge zimeagiza kuwa asilimia 60 ya makusanyo ya ndani
lazima zitumike katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo ndani ya halmashauri hizo hivyo lazima
viongozi hao wakawa makini katika mipango yao ya matumizi ya fedha hizo.








Post a Comment