![]() |
| Mabingwa wa U miseta kwa upande wa Mpira wa Miguu Halmashauri ya Kyela wakishangilia mara baada ya kuichabanga Halmashauri ya Mbeya 3.0 katika viwanja vya shule ya ufundi ya Iyunga. |
![]() |
| Kaimu Aisa Elimu Mkoa wa Mbeya Ndugu Jumma Mwaigombe |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Wito umetolewa kwa wakurugenzi Halmashauri za Mkoani Mbeya kuhakikisha
wanaendelea kulinda maeneo maalumu yalitengwa kwa ajili ya matumizi ya
michezo.
Aidha sanjali na kulinda maeno hayo pia wakurugenzi hao
wametakiwa kuacha tabia ya kutoa maeneo hayo kwa ajili ya wawekezaji .
Kauli hiyo imetolewa jijini Mbeya na Kaimu Afisa Elimu
Mkoa wa Mbeya Ndugu Jumma Mwaigambe wakati akifunga rasmi Mashindao ya Umiseta
ngazi ya Mkoa katika viwanja vya Shule ya Ufundi ya Iyunga.
Afisa Elimu huyo amesema kuwa kumekuwepo na tabia ya
baadhi ya viongozi katika halmashauri hizo ambao wamekuwa wakijiuhusisha na
uzaji wa maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya matumizi ya michezo.
Amesema maeneo mengi yaliyotengwa kwa ajili ya matumizi
ya michezo yamepokonywa na watu wanaodai kuwa ni wawekezaji huku viongozi wa
Halmashauri hizo wakiwa kimya bila kutoa kalipio u zuio hasa kwa kutokana na
kujali maslahi binafsi.
Aidha amedai kuwa zipo Halmasahuri ambazo zimeanzisha miradi ya maendeleo katika viwanja vya michezo hali ambayo imekuwa ikiwanyima fursa vijana kupata maeneo kwa ajili ya kuchezea mpira na michezo mingine.
Kufuatia hali hiyo Kaimu Afisa Elimu huyo amewataka
wakurugenzi hao kuhakikisha maeneo yote yalovamiwa na watu yanalejeshwa pamoja
na kuyaendeleza kwa ajili ya shughuli za michezo.
Katika Mashindano hayo teyari Mkoa wa Mbeya umekwisha
unda kikosi kitakacho shiriki katika mashindano ya Umiseta ngazi ya Kanda kwa
kushirikisha Mikoa ya Rukwa na Katavi.
Hata hivyo bingwa wa jumla wa mashindano hayo kwa michezo ya
jumla ni Mbeya jiji wakifuatiwa na Kyela katika mchezo wa Mpira wa miguu . .
Mwisho.














Post a Comment