![]() |
| Mmoja wa wadau wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Nuru Orphans Center kilichopo Uyole jijini Mbeya akikabidhiwa cheti kama sehemu ya shukrani kwa kuonyesha ushikirikiano kwa kituo hicho. |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Licha ya Asasi kuweka nguvu katika kusaidia shughuli
mbalimbali za kimaendeleo hususani jukumu la kulea watoto yatima Mkoani Mbeya bado serikali imetajwa kuwa nyuma
katika kuzisaidia asasi hizo.
Kauli hiyo imetolewa jijini Mbeya na Mkurugenzi wa wa
Asasi ya kiraia ya Nuru Orphans Center Ndugu Jasson Mark wakati sherehe za
kukabidhi vyeti na vitendea kazi kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu
ambao wamehitimu katika chuo cha Ufundi Veta jijini Mbeya kwa kufadhiliwa na kituo hicho.
Akizungumza amesema kwa asilimia kubwa ya watoto wanaolelewa katika kituo cha watoto yatima cha
Nuru Orphans Center wengi wao hulepelekwa
na serikali kupitia Idara ya Polisi na
Ustawi wa jamii.
Amesema pamoja na watoto na kituo hicho kuwapokea watoto
hao lakini bado serikali imekuwa
ikishindwa kutoa mchango wake kwa uongozi wa kituo hicho ili kusadia malezi
likiwemo suala la maradhi.
Amesema jukumu kubwa la kuwalea watoto hao limeachiwa kwa
viongozi na wanachama na baadhi ya wasamalia wema ambao wamekuwa wakijitoa katika
kutoa chakula na baadhi ya mahitaji mengine.
Hata hivyo amesema ubalozi wa Japani Nchini ulitoa msaada kwa
kituo hicho katika eneo la ujenzi wa Mabweni zaidi ya shilingi mil13 lakini bado halmashauri ya jiji la Mbeya imeshindwa kuwasilisha mchango huo.
Kufuatia hali hiyo
Uongozi wa kituo hicho umetoa wito kwa
serikali kuhakikisha inatoa ushawishi kwa Halmashauri za mkoa huo kuhakikisha zinaajiri watumishi
watakao kuwa na jukumu la kulea watoto yatima ili kupunga mzigo kwa vituo
hivyo.
Mwisho.













Post a Comment