Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mbunge jimbo la Mbarali CCM Mheshimiwa Dickson Kirufi mwenye suti nyeusi aliyesimama akiwa ndani ya kikao cha Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mbeya.

Wajumbe wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Mbarali wakifuatilia agenda za kikao hicho ambacho kilikuwa kikijadili suala la ushuru wa zao la Mpunga ambalo limekuwa kero kwa wakulima na wafanyabiashara wa eneo hilo.



Wananchi nao hawakuwa nyuma katika kikao hicho

Mbunge Kirufi akizungumza katika kikao hicho.




Mwananchi akiwa nje ya ukumbi kusubiri kusikiliza kikao.



Na EmanuelMadafa,mbeya

Katika hali isiyokua ya kawaida Baadhi ya Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya wameingia katika mgogoro na Mbunge wa Jimbo hilo Dickson Kirufi   mbele ya Mkuu wa Wilaya, Gulamhussein Kifu  katika kikao cha Baraza la Madiwani.

Hatua hiyo ilikuja baada ya Mbunge huyo  kuhoji malipo ya fedha za mawakala wa ushuru kwenye halmashauri hiyo wakati yeye ni mjumbe wa kamati ya fedha, mipango na uchumi ambayo ndiyo iliyohusika na jukumu la kuwapitisha mawakala hao.

Kikao hicho ambacho kilikuwa kikipitia , kujadili na kufafanua,ajenda moja ya suala la ushuru wa zao la mpunga ambapo hivi karibuni  kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya mawakala wa kukusanya ushuru wa mpunga na wakulima mashambani ambao wamekuwa wakigomea utaratibu huo.

Hatua hiyo ya madiwani kumzomea mbunge wao inadaiwa  ni kitendo  cha mbunge huyo kuhoji suala hilo, wakati yeye ni mjumbe wa kamati ya fedha , mipango na uchumi  ambapo alipaswa kufanya hivyo katika vikao  vya kamati na si kwenye baraza.

Baada ya mbunge huyo kupewa nafasi ya kuchangia hoja katika ajenda  hiyo ya ufafanuzi  kuhusu ushuru , katika hali isiyotarajiwa alianza kuuliza kama mawakala waliopewa tenda hiyo ya kukusanya ushuru wamelipa  malipo ya awali kama sheria inavyoagiza.

Hali hiyo ilionekana kuwakera madiwani hao ambao walianza kupaza sauti wakitaka Mwenyekiti wao kuwapa nafasi ya kutoa taarifa, jambo ambalo lilipuuzwa na Mwenyekiti huyo na kusababisha madiwani hao kuanza kuzomea.

Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Keneth Ndingo, alisimama na kuruhusu taarifa, ambapo diwani wa kata ya Itamboleo, lwitiko Mwangosi (CCM), alihoji sababu za mbunge huyo kuuliza swala hilo la malipo ya fedha za awali za mawakala wakati na yeye ni mjumbe wa kamati ya fedha.

Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa halmashauri alitumia kauli za busara kuwatuliza madiwani , huku akiendelea kutoa  nafasi kwa mbunge huyo kumalizia kuchangia  katika ajenda.

Wakitoa maazimio yao  katika ajenda hiyo, madiwani hao kwa pamoja waliazimia kusitishwa mara moja zoezi la ukusanyaji ushuru na kuweka utaratibu mpya wa namna ya kukusanya ushuru wa zao hilo, ambapo sasa ushuru wake utatozwa kwenye mchele na si mpunga.

Zoezi hilo la ushuru lililokuwa likitekelezwa na mawakala 10 , wanadaiwa kukiuka taratibu kwa kukusanya ushuru hadi kwa wakulima ambao walikuwa wakisafirisha mazao yao kutoka shambani kwenda kuhifadhi majumbani.

Walimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo kuitisha zabuni itakayowezesha kupatikana kwa mawakala wapya wanne watakaoendelea na kazi ya kukusanya ushuru huo
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top