Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi


 Na EmanuelMadafa,Mbeya
MWANAFUNZI  wa darasa la nne  Dorris Yuko mwenye umri wa miaka  12 amepoteza maisha  baada ya kubakwa na kisha kunyongwa shingo na binamu yake aitwaye Kenedy Elieza.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amesema tukio hilo limetokea juzi majira ya nne usiku katika Kijiji cha Matwebe Kata ya Kikole Wilayani Rungwe mkoani Mbeya.

Akielezea tukio hilo, Kamanda Msangi amesema, marehemu alikuwa amelala ndani na wadogo zake wawili katika nyumba ya bibi yao ambaye kwa wakati huo alikuwa amesafiri kuelekea Jijini Dar es Salaam.

Amesema, mtuhumiwa huyo ambaye ni binamu wa marehemu inasemekana alipitia dirishani kisha kuingia ndani ya chumba walicholala watoto hao na kufanya unyama huo.

Aidha, Kamanda Msangi amesema  inasemekana mtuhumiwa alifanikiwa kukimbia mara baada ya kufanya tukio hilo hivyo anatafutwa na polisi.

Wakati huo huo, Mwanafunzi wa kidato cha nne  Shule ya Sekondari  Mpanda Panda Pilly Kasebele(18) mkazi wa kijiji cha Ilundo Wilayani Rungwe, amepoteza maisha na kisha mwili wake kukutwa umetupwa kando kando ya barabara.

Mwili wa marehemu mwanafunzi huyo ulikutwa kando kando ya barabara hiyo mnamo tarehe 28/05/ 2014 majira ya tano za usiku katika Kijiji cha Kiwira Wilayani Rungwe.

Kamanda Msangi amesema kuwa , uchunguzi wa polisi umebaini kuwa marehemu huyo alikuwa akijaribu kutoa mimba.

Aidha, katika tukio hilo polisi linamshikilia Mwalimu wa shule hiyo Tukundonda Kiluswa(27) baada ya kuhusishwa na mauaji hayo.

Hata hivyo Kamanda Msangi alisema, Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi wa kitabibu na kutolewa kiumbe cha mtoto akiwa na umri wa miezi minne jinsi ya kiume.
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top