Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Wahitimu wa Chuo cha Academy Vocation Training Center wakiwa katika pozi la aina yake wakisubiri kukabidhiwa vyeti vyao vya uhitimu ngazi ya Cheti katika mafunzo ya Ukutubi na ujasilimali katika chuo hicho.
Mkurugenzi wa Chuo Cha Academy Vacation Traning Center Daines Mhoko akizungumza mbele ya wahitimu na wageni waalikwa katika sherehe za kuagwa kwa wanafunzi wa chuo hicho katika ukumbiwa mkapa jijini Mbeya

Wahitimu wakiserebuka kwa staili ya kwaito kufurahia sherehe hizo
Wageni waalikwa katika sherehe hizo


Na EmanuelMadafa,mbeya
Serikali kupitia wizara ya Elimu na Mfunzo ya Ufundi imetakiwa kubadilisha mfumo wa ufundishaji wa masomo ya Ukutubi ngazi ya cheti ili kuweza kuendana na mabadiliko ya sasa ya kiteknolojia na utandawazi uliopo sasa.

Kauli hiyo imetolewa na  wahitimu katika chuo cha Ufundi cha Academy Vocation Treaning Center kilichopo Kabwe jijini Mbeya wakati wakiti wakikabidhiwa vyeti vya uhitimu katika sherehe iliyofanyika katika ukumbi wa Mkapa jijini humo.

Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa vyeti hivyo baadhi ya  wahitimu hao wamesema kuwa kumekuwepo na changamoto kubwa katika usomaji wa masomo ya fani hiyo hasa kutokana na kusoma silabasi ambazo haziendani na wakati uliopo sasa.

Wamesema kuna baadhi ya masomo katika fani hiyo hususani katika uchapaji wamekuwa wakitumia mashine za kizamani (typewriting machine  ambazo kama wataajiliwa au kujiajili hawatoweza kuzitumia hasa kutokana na mfumo uliopo sasa wa Kidigiti zaidi.

Mmoja wa wahitimu hao Ndugu Edithar Nziku pamoja na Janeth Sanga wamesema shida kuwa ni pale mwafunzi anapo pata ajira na kukutana mazingira ambayo yamekuwa yakiwapa shida hususani kwa kukutana na vifaa vya kisasa vya ambavyo wao hawakupata fursa ya kuvisoma kipindi cha masomo yao.

Pamoja na kuwepo kwa chnagmoto hizo pia wanafunzi hao wamesema asilimia kubwa ya wanafunzi wanaomaliza katika chuo hicho wamkeuwa na mafanikio makubwa mara wanapo pata fursa ya kuajiliwa na hata kujiajili wenyewe hasa kutokana na kupewa mbinu mbalimbali za kiujasilimali na walimu wao.

Hata hivyo  kwa upande wake Mkurugenzi wa chuo hich
 Ndugu Daines Mhoka amesema kuwa changamto kubwa wanayokutana nayo katika hatua ya utoaji elimu kwa vijana hao ni uhaba wa baadhi masomo hususani somo la Typewriting pamoja kutopatikana kwa mashine hizo .

Aidha amesema kuwa changamoto nyingine ni uhaba wa maeneo kwa ajili ya kufundishia sanjali na ukosefu wa baadhi ya vifaa vya ufundishaji wa masomo ya fani hiyo.

Jumla ya wahitimu 30 ngazi ya cheti wamehitimu mafunzo katika chuo hicho na kupatiwa vyeti shughuli ambayo iliendana na sherehe katika ukumbi wa mdogo wa mkapa jijini Mbeya.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top