Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi


 Na EmanuelMadafa,mbeya
Mkazi wa kijiji cha Mantengu Wilayani mbozi Mkoani Mbeya Ndugu Wlliam Kabinji (38)  amekutwa ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kinachodhaniwa kuwa ni panga sehemu za usoni  na juu ya  jicho la kushoto kisha kunyongwa shingo na kutundikwa juu ya  mti akiwa amefungwa shingoni kwa kutumia  kitenge.

Tukio hilo limetokea June 08.06.2014 majira ya saa 12:00 mchana katika kijiji cha ilembo, kata ya vwawa, tarafa ya vwawa, wilaya ya mbozi, mkoa wa mbeya.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni kulipiza kisasi baada ya  marehemu kuchoma moto nyumba tatu za jirani zake  na kuiteketeza kabisa nyumba ya elias mwamlima (32) mkazi wa kijiji cha mantengu [a]  tarehe 04.06.2014 majira ya  saa 21:30 usiku na kutoroka.

Jitihada za kuwasaka na kuwakamata watu waliohusika na tukio hili ambao ni majirani wanaofahamika zinaendelea.

Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi ahmed z. Msangi anatoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na badala yake wajenge tabia ya kuwafikisha watuhumiwa wanaowakamata kwa tuhuma mbalimbali katika mamlaka husika kwa hatua zaidi za kisheria.
Mwisho

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top