Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya akifungua mkutano wa viongozi wa Mkoa na Wilaya na Halmashauri waliokutana kujadili utkelezaji  wa mfuko wa Afya ya Jamii( CHF) katika ukumbi wa Mikutano Hospital ya Mkoa jijini Mbeya.
Mjumbe wa ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya( NHIF)  Ndugu Charles Kajage akitoa salamu za Nhif katika mkutano huo.
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Nhif Kanda ya Nyanda za Juu kusini Dr.Mohamed Kiholile akitoa taarifa kwa viongozi hao juu ya utekelezaji wa Mfuko huo 
Wakuu wa Wilaya  Mkoa wa Mbeya wakiwa makini kufuatilia agenda za kikao hicho

Waganga wakuu wa Wilaya na jiji


Shughuli ya upimaji ukiendleea nje ya Kikao 
Meya wa jiji la Mbeya Atanas Kapunga 
Wadau wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro mara baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa mkutano huo .
 N a EmanuelMadafa,Mbeya

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, amesema miongoni mwa changamoto zinazokwamisha hamasa ya wananchi kujiunga na mifuko ya afya ya jamii ni huduma hafifu zinazotolewa na watoa huduma katika maeneo husika.

Mkuu huyo wa mkoa amesema hayo leo  jijini mbeya  katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa mfuko wa Taifa wa bima ya afya (NHIF) na mfuko wa afya ya jamii (CHF) Mkoa wa Mbeya na kujumuisha, wakuu wa Wilaya, wakurugenzi na wenyeviti wa Halmashauri na kufanyika katika ukumbi wa hospitali ya Mkoa kwa lengo la kujadili utekelezaji wa mfuko huo.

Amesema hadi kufikia Machi 31 mwaka huu ni kaya 89,841 tu ndizo zilizojiunga na na mfuko wa afya ya jamii  kati ya kaya 635, 037 zilizopo mkoani hapa, ambaya ni sawa na asilimia 14.15.

Amesema licha umuhimu wa mfuko huo kwa afya za jamii, mara kadhaa kumeibuka malalamiko yanayoelekezwa kwa watoa huduma , ambapo wananchi waliojiunga hulalamikia lugha mbaya, kutopatikana kwa dawa na vifaa tiba.
Amefafanua kuwa  changamoto hiyo  kwa ujumla imechangia kwa kiasi kikubwa kuwakatisha tamaa wananchi, hivyo hata  kukwamisha kabisa  malengo yaliyowekwa na serikali kuwa ya kufikia 30 ya watanzania wote kufikia 2015.
Kandoro amesema, kwa upande wa mradi wa afya ya mama na mtoto muitikio umekuwa ni mkubwa  kwani hadi kufikia sasa zaidi ya familia 70,000 , hivyo kuendelea kunufaika na mradi huo.

Meneja wa kanda ya nyanda za juu wa mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF), Dk. Mohamed Kiholile, alisema utekelezaji  wa mfuko huo kwa mkoa wa Mbeya bado si nzuri.

Amesema takwimu zinaonesha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi ndio inaongoza ambapo asilimia 21.42 wakazi wake wamejiunga, huku Halmashauri ya Busokelo ikiwa ya mwisho kwa uhamasishaji kwa wananchi kujiunga na mifuko hiyo kwa asilimia 4.15.

Amesema kwa halmashauri  ambazo mratibu wa NHIF na CHF ni mmoja  wateuliwe  wawili ili kuongeza ufanisi.

Naye Mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa mfuko wa taifa wa bima ya afya, Charles Kajege, aliwataka wakuu wa wilaya kuwa msitari wa mbele katika kuhamasisha na utekelezaji wa CHF na upatikanaji huduma bora katika vituo.
mwisho


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top