Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi


Na EmanuelMadafa,Mbeya

Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linawashikilia  Watu  26 kwa kosa la kunywa pombe kabla ya muda.

Watuhumiwa hao walikamatwa June26 mwaka huu  majira ya saa 09:30 asubuhi katika Mtaa Wa  tukuyu – Tunduma, Wilayani  Momba ,M koa wa mbeya katika msako mkali uliofanyika katika maeneo hayo.

Hata hivyo teyari watuhumiwa wote wamefikishwa mahakamani cc 26/2014.

Wakati huo Mkazi wa Nkuyu Ndugu Frank Mwampaja(40) anashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa mbeya akiwa na pombe kali [viroba] zilizopigwa marufuku na serikali.

Mtuhumiwa alikamatwa June 26 mwaka huu  majira ya saa 11:46 asubuhi katika eneo la Itungi-port, kata ya Buloma,  wilayani   kyela.
Mtuhumiwa alikamatwa akiwa na double punch katoni 2 na boss katoni 1. Taratibu za kumfikisha mahakamani zinaendelea. 

Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidzi mwandamizi wa polisi Ahmed z. Msangi anatoa wito kwa jamii na wafanyabiashara kwa ujumla kuacha kujihusisha na uuzaji na usambazaji wa pombe kali zilizopigwa marufuku na serikali kwani ni kinyume cha sheria na ni hatari kwa afya ya mtumiaji.

Aidha anatoa wito kwa jamii kutoa taarifa za watu/mtandao wa watu wanaojihusisha na uuzaji na usambazaji pombe kali zilizopigwa marufuku ili wakamatwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
Mwisho



Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top