![]() |
| Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
JUMLA ya Miradi 80 ya Maji inatekekelezwa mkoani mbeya
kwa mwaka 2013~14 katika vijiji 112 ambapo kati ya hivyo miradi 16 imekamilika.
Vijiji hivyo ni pamoja na
Namkukwe Wilayani Chunya Natambalala Wilayani Momba pamoja na Kyimo Wilayani Rungwe .
Vingine ni Kikuba
Busokelo na Ubaruku Chimala
Simike pamoja na Mbembe ,Masoko. Ikombe ,Maninga ,lwalanje na Igale .
Kwa mujibu wa Taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu
Abbas Kandoro imefafanua kuwa katika
miradi hiyo teyari 54 iko katika hatua mbalimbali za ujenzi na mingine 10 iko katika hatua za
mchakato wa Zabuni.
Amesema katika miradi hiyo 80 jumla ya shilingi bilioni 39.4 zinategemewa kutumika hali ambayo itainua kiwango cha upatikanaji wa
hudumza za maji kwa maeneo ya vijijini
na kufikia asilimia 71.8 .
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa wa Mbeya mkoa wa mbeya
unajumla ya miundombinu ya maji 1,331 pamoja vituo vya kuchotea 5,171 ambapo
hadi kufikia mwezi mwaka huu asilimia 56.2 wanapata huduma ya maji.
Mwisho







Post a Comment