Maafisa nchini India wamesema wanahofu kuwa zaidi ya watu 130
wamenasa kwenye kifusi cha jengo lililoporomoka kusini mwa India,takriban Watu
watano wameripotiwa kupoteza maisha katika tukio hilo mjini Porur.wengi wa
walionasa wanaaminika kuwa wafanyakazi waliokuwa wakijenga jengo la ghorofa 11.
Kikosi
ha uokoaji kinafanya jitihada za kuokoa walioathiriwa na ajali hiyo. siku ya
jumamosi, watu 10 ,miongoni mwao watoto watano, walipoteza maisha mjini
Delhi,baada ya jengo la makazi ya watu kuporomoka.
India
imekua ikikumbwa na matukio ya kuporomoka kwa majengo, sababu ikielezwa kuwa
usalama usio madhubuti na ujenzi usiozingatia viwango bora.
Mwezi
Januari mwaka huu, takriban watu 14 walipoteza maisha baada ya jengo lililokuwa
kwenye hatua za ujenzi kuporomoka katika jimbo la Goa.BBC SWAHILI
Takriban
watu 42 walipoteza maisha baada ya kuangukiwa na Jengo la ghorofa nne mjini
Mumbai mwezi Septemba mwaka jana.
Post a Comment