![]() |
| Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Mbeya Ndugu Amani Kajuna mwenye miwani akiwa pamoja na kamati ya utekelezaji Uvccm Mkoa wa Mbeya katika Mkutano na Waandishi wa Habari |
![]() |
| Muda wa Maswali kwa Waandishi wa Habari |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Baraza la kuu la Umoja wa Vijana( Uvccm) Mkoa wa Mbeya, linakutana
jijini Mbeya na kujadili mambo kadhaa likiwemo suala la
uchaguzi ujao wa serikali za Mitaa unaotalajiwa kufanyika hivi karibuni .
Mbali hilo pia umoja huo
upo katika maandalizi ya mwisho kwa
ajili ya kuwasimika makanda 11 wa vijana ikiwa ni moja ya utekelezaji wa
mikakati iliyojiwekea chama kwa kila mwaka.
Akizungumza na waandishi
wa habari jijini Mbeya Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Mbeya Ndugu Amani Kajuna
amesema uchaguzi wa serikali za mitaa ndio
sehemu ya misingi ya siasa kwa chama chochote kile kujipima.
Amebainisha kuwa baraza
hilo litatumia kikao hicho kujadili na kupanga mikakati ili kuona ni
jinsi gani watakavyo ibuka na ushindi mkubwa katika chaguzi hizo sanjali na
uchaguzi ujao 2015..
Aidha Mwenyekiti huyo
amefafanua kuwa katika kuelekea katika chaguzi za serikali mitaa ndio misingi
mikuu ya vyama ifikapo kwenye uchaguzi mkuu hivyo mikakatia hivyo
kama mikakati ya umoja huo itakuwa mizuri chama cha mapinduzi kianuwezo wa
kuyarudisha majimbo yote yaliyochukuliwa na upinzani.
Aidha Kajuna amesema
kuwa mbali na kujadili suala la chaguzi za serikali za Mitaa pia Baraza hilo
litajadili mstakabali wa Taifa hasa
katika harakati za upatikanaji wa Katiba mpya.
Hata hivyo Kajuna
ameweka wazi juu ya usimikwaji wa Makamanda 11 ambao unatalajiwa kufanywa julai 6 mwaka
huu sherehe ambazo zitafanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya na
kuhudhuliwa na Meya wa Jiji la Ilala
Jerry Slaa.
Amesema wao kama vijana wanapaswa kuwekana sawa hasa kipindi
hiki ambacho nchi inatarajia kupata Katiba mpya kwa kuhakikisha wanajipanga na
kusimama imara ili kuhakikisha kuwa ujio
huo wa katiba hauthiri nchi kama ilivyotokea maeneo mengine.











Post a Comment