|
Na EmanuelMadafa
Timu ya soka ya taifa ya
Tanzania, Taifa Stars imefungwa mabao 4-2 na wenyeji, Botswana leo mjini
Gaborone katika mchezo nwa kirafiki. Mabao ya Stars yalifungwa na Khamis Mcha
'Vialli' na John Bocco 'Adebayor' kwa penalti.
|
Mechi imefanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Gaborone ni sehemu ya
maandalizi ya Taifa Stars kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika dhidi ya
Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Stars
inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inatarajiwa kurejea nchini Julai 6
mwaka huu kuendelea na programu nyingine kwa ajili ya mechi dhidi ya Msumbiji.
mwisho







Post a Comment