Waziri wa Nchi ofisi ya waziri Mkuu (uwekezaji na uwezeshaji) Daktari Mary Nagu akizungumza katika kongamano hilo |
Mmoja wa wadau wakubwa katika sekta ya uwekezaji wa pili kulia Mzee Mzindakaya akiwa makinini kufuatilia yanayojili katika kongamano hilo |
Mkuu wa Mkoa wa mbeya Abbas Kandoro akitoa salama za Mkoa katika Kongamano hilo |
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Christina Ishengoma akitoa salama za Mkoa wa Iringa katika kongamano hilo |
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipiga picha ya pamoja na baadhi ya wawekezaji waliohudhuria Kongamano hilo katika ukumbi wa Mikutano wa Mkapa jijini Mbeya. |
Picha ya pamoja ya Waziri Mkuu na Viongozi mbalimbali |
Na
EmanuelMadafa,Mbeya
WAZIRI
Mkuu, Mizengo Pinda, ametoa saa 12 kwa uongozi wa Shirika hodhi la mashirika ya
umma nchini (CHC) kufika mkoani Mbeya, ili kumpatia sababu zilizosababisha
kushindwa kupatikana kwa mwekezaji katika kiwanda cha kusindika nyama cha
Mbeya.
Waziri
Pinda ametoa agizo hilo leo jijini Mbeya wakati wa kongamano la
uwekezaji la kanda ya nyanda za juu kusini,kwa kummuagiza Waziri
wa nchi , Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji,Dk. Mary
Nagu, baada ya viongozi wa shirika hilo kukosekana ukumbini ili kutoa maelezo.
Kutokana
hali hiyo, alimtaka Dk. Nagu kuwasiliana na wawe wamefika mkoani humo
leo jioni ili wakutane naye na kumpatia maelezo ya kina
juu ya sababu zinazosababisha kukosekana kwa mwek,ezaji katika kiwanda hicho.
Waziri
Mkuu Pinda yupo mkoani humo kwa ziara ya ya kikazi ya siku mbili, ambapo leo
amefunghua kongamano hilo la uwekezaji na kesho anatarajia kuzindua
maonesho ya wakulima ya Nanenane kwa mikoa hiyo.
Agizo
hilo la Pinda kufufuliwa kwa kiwanda hicho ni la pili, ambapo mwaka
2011 alipofanya ziara mkoani hapa, alitoa miezi 6 kwa viongozi wa CHC
wahakikishe wampata mwekezaji na kiwanda hicho kuanza kazi.
Akiwahutubia
wadau hao wa sekta ya uwekezaji , Waziri Mkuu Pinda alisema mikoa ya Nyanda za
juu kusini ina fursa kubwa katika sekta hiyo tena kwa kuwatumia wawekezaji wa
ndani.
Pinda
amesema kufufuliwa kwa kiwanda hicho kitawanufaisha wananchi wengi , hususani
vijana kupata ajira.
Aidha,
Waziri pinda, alishangazwa na kitendo cha watendaji wa shirika hilo
kutohudhuria kongamano hilo ambalo linanafasi kubwa ya kutoa fursa kwa
wewekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza hali itakayosaidia kukua kwa uchumi
na maendeleo kupatikana.
Kiwanda
cha kusindika nyama cha Mbeya ni miongoni mwa viwanda kadhaa vilivyokufa na
kusababisha tatizo kubwa la ajira hususani kundi la vijana.
Akitoa
maelezo katika ziara ya awali ya Pinda mkoani hapa, mwaka 2011,
ofisa wa kiwanda chja nyama Mbeya, Joseph Mapunda, alisema ujenzi wa kiwanda
hicho ulianza mwaka 1975 na ulikamilika na kuanza kazi mwaka 1985 .
Mwisho.
Post a Comment