Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Kaimu Meneja wa Kampuni ya Seed Co Tz Ltd Ndugu Michael Rikanga akionyesha moja ya fomu zitakazotakiwa kujazwa na washiriki  kutoka katika shule mbalimbali za msingi katika mkutano wake na waandishi wa Habari leo jijini Mbeya.

Waandishi wakiwa makini kufuatilia mkutano huo




Na Emanuel Madafa,Mbeya
Katika kuhakikisha serikali inatimiza azma yake ya kuwakomboa wakulima nchini hususani katika suala la kilimo bora cha kibiashara  taasisi binafsi zinazojiuhusisha na shughuli ya usambazaji  wa  mbegu bora za kilimo zimeendelea na harakati za kuisaidia serikali katika suala hilo.

Hatua hiyo ni pamoja na kutoa elimu pamoja na kusambaza pembejeo bora za kilimo zenye kukidhi mahitaji ya mkulima.

Kutokana na hali hiyo kampuni ya Seed  Co imezindua shindano  rasmi la mashamba darasa  kwa shule za Msingi Tanzania ambazo zitaanza mchakato wa kulima shamba darasa  kwa kufuata kanuni bora za kilimo cha kisasa .

Akizungumza jijini Mbeya Kaimu meneja wa Kampuni hiyo Kanda ya Nyanda za juu Kusini Ndugu Michael Rikanga amesema  shindano hilo ni mahususi kwa shule za msingi za Mbeya  Iringa Njombe na Ruvuma pamoja na Rukwa na Katavi ambapo shindano hilo linatalajiwa kuanza msimu mpya wa kilimo  .

Amesema kwa shule itakayokuwa imelima shamba darasa zuri kwa kuzingatia misingi yote ya kilimo bora cha kisasa itajishindia zawadi kubwa ya madawati yenye thamani ya shilingi mili15.
Amesema  pamoja na  zawadi hiyo ya madati kwa mshindi wa kwanza pia mshindi atapatiwa  sare za michezo  madaftari na kalamu za kuandikia pamoja na mwalimu wa somo la kilimo kupatiwa simu ya mkononi.

Amesema ili kushiriki mwanafunzi au mwalimu wanatakiwa kutembelea maduka ya mawaka maalum waliothibitishwa na Kampuni hiyo ya Seed Co ili kujisajili katika shindano hilo.
Hata hivyo Meneja huyo amesema kuwa katika hatua za uandaaji na usimamizi wa shamba darasa Kampuni hiyo itatoa pemebejeo zote zitakazohitajika  ikiwa ni pamoja na mbegu za mahindi mbolea ya kupandia na kukuzia .

Mahitaji  mengine ni pamoja na madawa ya kupulizia iwapo iwapo mazao yataonyesha dalili za kushambuliwa na wadudu waharibifu.

Lengo la kampeni hiyo kufundisha kilimo  kwa njia ya vitendo  kwa wanafunzi  wa shule za msingi sanjali na kutoa  nafasi kwa wanafunzi kujishindia zwadi kutoka katika kampuni hiyo ya Seed Co Tanzania Limited.

Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top