Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Naibu  Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Godfrey Zambi.

Na Emanuel Madafa,Mbeya
SERIKALI   inatarajia kununua tani 200,000 za mahindi, huku ikifanya jitihada za kutafuta masoko zaidi nje ya nchi ili kuhakikisha wakulima wote wanauza kwa tija.

Kauli hiyo imetolewa Naibu  Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Godfrey Zambi, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kutembelea vituo vya wakala wa hifadhi ya taifa ya chakula (NFRA) Wilayani Ileje Mkoani Mbeya.

Amesema, lengo la serikali ni kuhakikisha inanunua mazao yote ya mahindi kutoka kwa wakulima hivyo mbali ya kuchukua tani hizo pia inaendelea na mikakati ya kutafuta masoko ya nje ili kuhakikisha wakulima wanauza zao hilo kwa faida.

Amesema licha ya  serikali kutokuwa na uwezo wa kuchukua mahindi yote yaliyopo mikononi mwa wakulima nchini, bado inaendelea na jitihada za kutafuta masoko nje ya nchi.

Amesema, wakulima wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanahifadhi mahindi ili yawe na ubora utakaolingana na bei inayotolewa, lakini pia kuvutia masoko ya nje ya kimataifa).

Aidha, Zambi, amewataka wakulima hao kutokubali kurubuniwa na wachuuzi ambao hivi sasa wananunua bei ya mahindi kwa shilingi 5000 hadi 6000 kwa debe wakati serikali inanunua mahindi hayo kwa shilingi 9000 kwa debe, bei ambayo haiwezi kupatikana katika soko lingine ndani na nje ya nchi.

Aidha, kwa upande wake,Meneja Kanda ya Makambako wa NFRA, Abdulahi Nyangasa, amewataka watendaji na watumishi wa wakala, kuhakikisha wanakagua mizigo yote ya mahindi ambayo inawaslishwa kwenye vituo hivyo, huku akiwasisistiza wakulima kuhakikisha wanachambua mahindi  kabla ya kuyafikisha vituoni.

Aidha  amesema wakala hao wa hifadhi ya taifa ya chakula mwaka jana ilinunua zaidi ya tani 16000 za nafaka katika kituo cha Mbozi, ambapo mwaka huu inatarajia kununua zaidi ya tani 15000.


Mwisho


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top