Na EmanuelMadafa,Mbeya
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, ameziagiza halmashauri zote
mkoani Mbeya kuwachukulia hatua za kinidhamu watendaji watakabaoinika kuwa
chanzo cha kuzalisha hoja za ukaguzi zitakazobainishwa na Mkaguzi na Mdhibiti
wa fedha za Serikali (CAG).
Amesema hatua hiyo ni kutokana na uzembe wa utekelezaji wa miradi ya
maendeleo kwenye idara zao.
Kandoro ametoa agizo hilo kwenye kikao Maalum cha Baraza la
Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kilichoandaliwa kwa ajili ya
kupitia hoja za ukaguzi wa hesabu za fedha za halmashauri hiyo ambapo katika
taarifa hiyo hoja 80 hazijapatiwa ufumbuzi.
Amesema kuwa ofisi yake haitavumilia tabia ya watendaji kuzalisha
hoja kutokana na uzembe na hivyo ameagiza Mabaraza ya Madiwani kuanza kuchukua
hatua dhidi ya watendaji hao na taarifa ya hatua hizo za kinidhamu itolewe
kabla ya kufanyika vikao vya kupitia hoja za ukaguzi.
Amesema ikiwa hatua stahiki hazitachukuliwa dhidi ya watendaji
hao, itabidi viongozi wenye dhamana ya kuwachukulia hatua na wao wawajibike
kutokana na kulea uzembe kwenye maeneo yao.
Agizo hilo la Mkuu wa Mkoa lilitokana na Taarifa ya ukaguzi ya
Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kuonyesha kuwa licha ya halmashauri
hiyo kupata hati safi ya ukaguzi, lakini kulikuwepo na hati chafu katika mradi
wa maji.
Amesema kuwa hati hiyo chafu kwenye mradi wa maji inaitia doa
halmashauri hiyo, hivyo kuagiza watendaji wanaosababisha kuwepo kwa hati chafu
kwenye idara yao washughulikiwe.
Hata hivyo Kandoro aliipongeza Halmashauri hiyo kwa kupata hati
safi ya ukaguzi pamoja na kuongoza kwa makusanyo ya mapato ya ndani
ikilinganishwa na Halmashauri zote mkoani Mbeya.
mwisho
Post a Comment