Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na EmanuelMadafa,Mbeya

KIKONGWE cha miaka 70, kimeuawa kwa kupigwa risasi aina ya SMG maeneo ya mkono wa kushoto chini ya bega na kupelekea kifo chake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alisema tukio hilo limetokea jana, majira ya saa tisa za usiku katika eneo la Soweto, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Sisimba Jijini Mbeya.

Amemtaja marehemu huyo kuwa ni Nkusubila Kaminyonge (70) mkazi wa eneo la Soweto lililopo Jijini Mbeya.

Akielezea  tukio hilo, Kamanda Msangi, alisema  inadaiwa kuwa wauaji hao, walivunja geti la nyumba ya marehemu huyo kisha kuingia ndani na kutekeleza unyama huo.

“Inadaiwa kuwa, watu hao walivunja geti la nyumba na kisha kuingia ndani na kuvunja mlango wa chumba alichokuwa amelala marehemu na kumpiga risasi”alisema Msangi.

Amesema, kuwa wakati watu hao wakifanya unyama huo, imeelezwa kwamba marehemu alikuwa amelala ndani na  mume wake aitwaye Osia Malambugi(72) mkazi wa Soweto Jijini Mbeya.

Amesema, kwa mujibu wa maelezo kutoka kwa mzee huyo, inadaiwa kuwa mara tu ya watu hao kufyatua risasi mzee huyo alishtuka baada ya kusikia mlio mkubwa wa risasi na kukuta mke wake amepigwa.

Aidha, Msangi, amefafanua kuwa, inasemekana kwamba wauaji hao mara baada ya kufanya tukio hilo walifanikiwa kukimbia.

Hata hivyo, amesema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa watu hao hawakuchukua kitu chochote na kwamba askari wanaendelea na upelelezi wa mauaji hayo.


Mwisho.   

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top