Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Uingereza imeondoa tahadhari iliyokuwea imetoa kwa raia wake dhidi ya Kusafiri Kenya.
Tahadhari hiyo kwa ukubwa likuwa inalenga maeneo ya mitaa ya mabanda, na baadhi ya maeneo ya Pwani ambako ilihofiwa kuwa raia wa kigeni wanalengwa kwa mashambulio ya kigaidi.
Hatua hiyo ya kuondolewa tahadhari kwa raia wa Uingereza kusafiri Kenya, inaanza kutekelezwa mara moja.
Tahadhari hiyo ilikuwa imewekwa baada ya machafuko yaliyotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu yapata miaka saba iliyopita.
Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza imewasiliana na wizara ya ndani ya nchi hiyo kwamba hali ya hatari imeshuka kwa kiasi kikubwa.
Wizara hizo zimesema kuwa tahadhari kama hizo hutolewa kuambatana na sera za nchi hiyo za kuwatolea usalama raia wake kote duniani licha ya taifa linalozungumziwa.
Serikali ya Kenya ilikuwa imelalamika kuwa tahadhari kama hizi zinazotolewa na mataifa ya Magharibi hazina msingi na zinaathiri uchumi wa nchi hiyo.BBC SWAHILI

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top