Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt Nouman Sigalla ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya  akizungumza na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo katika kituo cha Afya  Mwanjelwa jijini hapa.
Dkt Sigalla akitoa chanjo wa mmoja wa watoto kama sehemu ya uzinduzi wa Chanjo hiyo





Mwakilishi wa Jambo leo Ndugu Venance Matinya akijianda kupatiwa chanjo.







Meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga
Mkurugenzi wa jiji la Mbeya Mussa Zungiza


Kampeni ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imezunduliwa rasmi leo jijini Mbeya ambapo kimkoa kampeni hiyo imefanyika  Wilayani Ileje mkoani hapa.

Pia  kampeni hiyo  itawahusisha watoto wenye umri wa kuanzia miezi 9 hadi miaka 15.

Aidha kampeni hiyo itaambatana na utoaji wa matone ya Vitamini A, dawa za kutibu na kukinga magonjwa ya Minyoo, Usubi,Matende na Mabusha. 


Pia  lengo na madhumuni ya kampeni hiyo ni kudhibiti milipuko ya magonjwa ya Surua na Rubella ili kupunguza vifo na madhara yanayosababishwa na magonjwa hayo..


Chanjo ya Surua na Rubella itatoa fursa ya kutoa kinga kwa watoto wengi zaidi ambao hawakupata chanjo hiyo utotoni katika mikoa yenye maambukizi makubwa ya magonjwa hayo ambayo ni Mtwara, Lindi, Tanga , Dar  es salaam,Morogoro, Pwani, Tabora, Manyara, Iringa, Ruvuma, Rukwa, Katavi, Singida, Dodoma na Njombe.


 Surua na Rubella itatolewa kwa watoto wenye umri wa miezi 9 hadi chini ya miaka 15, matone ya vitamin A kwa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi chini ya miaka 5.

Nyingine ni dawa za minyoo (Mebendazole) zitakazotolewa kwa watoto wenye umri wa miezi 12 hadi chini ya miaka 5 nchi nzima na dawa za kutibu na kukinga minyoo (Albendazole) Usubi, Matende na mabusha au Ngirimaji kwa watu wenye umri wa kuanzia miaka 5 na kuendelea katika mikoa 16 iliyobainishwa.


Katika uzinduzi huo wito umetolewa  kwa wazazi na walezi  kuhakikisha kuwa wanawapeleka watoto wao katika vituo vya afya ili waweze kupata chanjo  hiyo.


Pia ametolewa wito kwa mama wajawazito kuhakikisha kuwa wanapata chanjo ya Surua-Rubella ili kuwakinga watoto wao dhidi ya matatizo ya Moyo, mimba kuharibika, kujifungua kabla ya wakati na mtindio wa ubongo yanayotokana na ugonjwa huo.


Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top