Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na Mwandishi wetu.
MCHEZO wa ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Tanzania Prisons na Simba uliochezwa jana katika uwanja wa Sokoine Jijini hapa, uligubikwa na vituko kadhaa vilivyoambatana na hisia za kishirikina.
Hali hiyo ilitokea pale Simba walipoamua kuvunja utaratibu wa kuingia katika vyumba vya kubadilishia, kufuatia kukataa kupitia njia yao na badala yao kupita walikopita timu ya Tanzania Prisons.

Wachezaji wa Simba walifikia maamuzi hayo baada ya kupokea amri kutoka kwa mtu mmoja aliyewapa maelekezo baada ya kukaribia eneo hilo la vyumba vya kubadilisha vilivyopo chini ya jukwaa Kuu ndani ya Uwanja wa Sokoine.
Mtu huyo ambaye hata hivyo hakuweza kujulikan a mara moja kama alikuwa ni kiongozi wa timu hiyo, kabla timu hiyo haijafika ndani ya uwanja alionekana kusimama katika eneo hilo na alipoona wachezaji wa Simba wanaingia uwanjani alijitayarisha na kuzuia njia ya kuingilia Simba.

Mtu huyo ambaye muda wote alionekana kusimama kwa ukakamavu wa hali ya juu baada ya kuona wachezaji wa Simba wamekaribia eneo hilo lakuingilia katika vyumba vya kubadilishia nguo alionekana kuwatolea ishala wachezaji akiwaelekeza kupitia upande wa pili huku yeye akiziba njia.
Kutokana na hali hiyo wachezaji hao wa Simba walitii amri hiyo na kuamua kupitia njia walioitumia Tanzania Prisons kuingilia katika vyumba hivyo vya kubadilishia na kasha mwenye kuondoka na kutokomea kwenye jukwaa Kuu.
Katika hatua nyingine , wachezaji wa Simba katika mchezo huo wakitumia lango Kuu la uwanja wa Sokoine waliingia wakiwa chini ya ulinzi mkali wa watu wanaodhani kuwa ni makomandoo wakiyasindikiza magari mawili.

Hata hivyo, Simba waliingia uwanjani hapo wakiwa kwenye gari  aina ya Coaster , huku gari ambalo hulitumia siku zote likiwa mbele na watu wacheche ambao walionekana ni mashabiki.
Simba tangu wafike Jijini hapa kujiwinda na mchezo huo walionekana kuwa  makini sana na suala la hujuma, ambapo inadai waliamua kukodi Hoteli yote wakihofia hujuma za aina yeyote.
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top