Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, asiye na Wizara Maalum, Profesa MarkMwandosya akizungumza na waandishi wa habari jijini mbeya.
 
Na EmanuelMadafa,Mbeya 
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, asiye na Wizara Maalum, Profesa MarkMwandosya,ameshangazwa na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakitumia fedha katika kutafuta nafasi mbalimbali za uongozi na kuhoji ya kwamba fedha hizo wanazitoa wapi na kwa maslahi ya nani.

Amesema yeye ni maskini hana fedha za kuwanunua wajumbe wa kumpigia kura ifikapo mwaka 2015 lakini ameweka bayana kwamba yupo tayari kuwatumikia wananchi kwa uadilifu mkubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kumaliza  kikao cha Baraza la  CCM Mkoa wa Mbeya, kilichokuwa kikipitia na kujadili masuala mbalimbali ya chama kilichofanyika katika ofisi za CCM zilizopo Jijini humo.

Amesema, hivi sasa kumeibuka  mtindo na imani kwamba fedha ndio msingi  wa uteuzi na kuchaguliwa kwa mtu kuwa kiongozi, jambo linalomtatanisha sana na kwamba ni kinyume cha misingi na matarajio ya wananchi na ya vyama vya siasa.

Amesema, wananchi wanafahamu mshahara wake, tangu alipoteuliwa kuwa Waziri hadi sasa na wanaweza wakaongeza na zile za safari zake zote alizosafiri lakini hana jeuri ya  kuwalipa wajumbe ili wampigie kura.

Amesema, endapo nafsi yake itamsukuma kuwatumikia wananchi basi itakuwa ni kwa upendo wake  lakini si kwasababu  ya kwamba yeye anafedha na angependa  kutangaza kwamba fedha hizo hana ila yeye matumaini yake makubwa ni hali aliyokuwa ambayo inatokana na kuafanana na wananchi.

Amesema, ni vema wahusika hao wakazielekeza fedha hizo kwa wananchi kwa kuwapatia thamani halisi kupitia kwenye hospitali na vituo vya afya kwa matumizi ya dawa na kununua mabati dawa , vituo vya afya kuwekewa mabati kuliko kushusha thamani ya mtu na kumfanya mtumwa kupitia fedha zako.

Amesema, wakati umefika kwa jamii kurudi kwenye siasa za kizamani  kuliko kumrubuni mwananchi kwa uongozi kupatikana kwa njia ya fedha, fedha ambazo hujui zimetoka wapi na zitarudishwa kwa njia ipi.

Amesema, siasa ya sasa imekuwa ni ya watu wenye fedha au watu waliogeuzwa mawakala kutokana na fedha za watu fulani bdala ya siasa ya wafanyakazi na wakulima  ambayo ndiyo iliyokuwa ikipiganiwa na Mwalimu pamoja Karume.

Hata hivyo amesema nivema kutambua kuwa hatua ya kumchagua mtu kuwa rais kupitia chama cha Mapinduzi ni hatua ngumu sana kwani huyo ndiyo anayetegemewa kuwa mwenyekiti wa chama hicho hivyo si suala la kukurupuka tu.
 
Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top