Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na Mwandishi wetu,

Mtoto  umri wa mwaka mmoja na nusu [011/2] aliyetambulika Ndugu  Elisha Juma mkazi wa shewa amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye kisima chenye maji machafu.
           
Tukio hilo limetokea Octob 23 mwaka huu majira ya saa 07:00 asubuhi katika Mtaa  shewa, kata ya mwakibete jiji  mbeya.

Inadaiwa kuwa, kabla ya tukio hilo, marehemu alikuwa akicheza maeneo ya jirani na kisima hicho kilichokuwa na maji machafu ya mvua yaliyokuwa yamehifadhiwa kwa ajili ya shughuli za ujenzi.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa mbeya kwa ajili ya uchunguzi wa kitabibu.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidizi wa polisi Barakael Masaki anatoa wito kwa wazazi walezi kuwa makini na watoto wadogo ikiwa ni pamoja na kuweka uangalizi wa kutosha ili kuepuka madhara yanayoweza kuepukika.

Aidha, anatoa wito kwa jamii kufukia mashimo, kufunika visima na matundu ya maji machafu kwani ni hatari kwa watoto wadogo.

Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top