Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Mtanange unaosubiriwa kwa hamu kubwa na wakazi wa Mkoa wa Mbeya kati ya  timu za Simba Fc na Tanzania Prisons, ambao unaotalajiwa kutimua vumbi  ndani ya uwanja wa sokoine 0ctoba 25 mwaka huu mchezo huo  umeendelea kuchukua sura mpya  katika vitongoji vya jiji la mbeya ambapo mpaka sasa timu hizo zimegoma kuutumia uwanja huo  wa sokoine kwa ajili ya mazoezi kutokana na sababu zisizoeleweka.

Timu ya Simba, imewasili Jijini Mbeya juzi, kwa kutumia usafiri wa ndege na kufikia  hotel ya Padz , imedaiwa kugoma kuutumia uwanja wa Sokoine kwa ajili ya mazoezi na kutafuta kiwanja kingine.

“Timu ya Simba Fc, imewasili  Mbeya juzi na kufikia hotel ya Padz na kwamba siku (leo) kwa utaratibu wa TFF inatakiwa kuutumia uwanja wa Sokoine kwa mazoezi lakini hatuta utumia  kutokana na sababu za kiufundi,”kilisema chanzo hicho cha habari ambacho kiliomba kutoandikwa jina lake.

Kilisema,  mwenendo  wa timu  hiyo bado haujakaa vizuri  kutokana na kutoa sare nne ndani ya mechi nne hivyo ni vema ikajiwekea ulinzi wa kutosha katika kutafuta pointi tatu ambazo ndizo zimewaleta Mbeya.

Aidha, kwa upande wa timu ya Tanzania Prisons, imeelezwa,  licha ya timu hiyo kuwa wenyeji wa uwanja huo lakini nao wameonekana kutoutumia uwanja huo kufanyia mazoezi kwa maelezo kwamba ndio desturi yao kutokana na kutumia kiwanja chao kilichopo ndani ya Jeshi la Magereza.

“Sisi hatuna sababu ya kutumia uwanja wa Sokoine kwa mazoezi kwani tumekuwa na kiwanja chetu ambacho tunakitumia mara kwa mara lakini hii haituzuii kukilinda kiwanja hiki ,”alisema John Mwakitange mdau wa timu ya Tanzania Prisons.

Amesema, timu yetu kwa sasa imepoteza mvuto kwa mashabiki wetu kutokana na kuruhusu kufungwa na Ruvu Shot , hivyo mechi dhidi na Simba ni lazima tujipange kwa kila njia ili kuhakikisha  tunawarudisha mashabiki wetu pamoja na kutokubali kuvunja rekodi tuliyonayo juu ya Simba hasa timu ikiwa nyumbani.

Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top