Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwenyekiti wa zamani wa Simba SC, Ismail Aden Rage amekanusha tetesi kuwa amekuwa akiihujumu timu hiyo ili ifanye vibaya kwenye mechi zake. Kupitia Kikaangoni Live ya EATV, Rage alisema akiwa kama shabiki mkubwa wa Simba aliyoitumikia kwa muda mrefu, hawezi ili ipate matokeo mabovu.
“Kusema kweli siwezi kuihujumu timu yangu Simba nadhani mimi nimeitumikia kuliko watu wengine wengi tu hapa na pia hapa nilipofika kwa sasa Simba wana mchango wao mkubwa tu hivyo siwezi kuihujumu Simba,ila nachoweza kusema ni kwamba mashabiki pamoja na uongozi wa Simba uliopo madarakani sasa katika mpira kuna mambo matatu kushinda sare au kufungwa kwa hiyo tukubali haya matokeo,pia tuwape muda huenda timu ikabadilika mbele ya safari,” alisema.
Hivi karibuni Simba iliwasimamisha wachezaji wake watatu, Shabani Kisiga, Amri Kiemba na Haruna Chanongo kutokana na kudaiwa kuchangia matokeo mabovu ya timu hiyo.

Hata hivyo Rage alisema hafikirii kugombea nafasi yoyote kwenye klabu hiyo. “Sijafikiri kugombea nafasi ya Rais katika Klabu ya Simba kwani nahitaji kupumzika,sasa hivi uongozi wa simba ni mgumu sana,” alisema.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top