Na EmanuelMadafa,Mbeya
WANANCHI wa Kijiji cha Ngyekye Wilayani Kyela Mkoani Mbeya, wamejikuta wakitafuna kitoweo cha nyama ya mbwa baada ya kuuziwa mishikaki kutoka kwa mfanyabiashara Ahadi Jesikaka(20).
WANANCHI wa Kijiji cha Ngyekye Wilayani Kyela Mkoani Mbeya, wamejikuta wakitafuna kitoweo cha nyama ya mbwa baada ya kuuziwa mishikaki kutoka kwa mfanyabiashara Ahadi Jesikaka(20).
Tukio
hilo limetokea Nov4 mwaka huu majira ya saa saba za mchana, katika kijiji cha Ngyekye
Kata ya Matema Wilayani Kyela.
Wakizungumza na blog hii kwa njia ya simu muathirika wa tukio hilo, Anyandwile
Mbwilo, alisema hali hiyo imetokea baabda ya kufika kwenye kibanda cha
mfanyabiashara huyo na kuagizia chakula kilichoambatana na nyama
iliyotengenezwa mithili ya mishikaki.
“Nilifika
kwenye kibanda cha chakula kinachomilikiwa na Jesikaka na kuagiza chipsi
zilizoambatana na mishikaki baada ya kumaliza kula nilimsikia mmiliki huyu
akitoa kauli za ajabu, akidai kwamba “Eti mnajidai hamli mbwa mbona leo mmekula”alisema
.
Amesema,
baada ya kusikia kauli hiyo yeye pamoja na baadhi ya wateja wa;liokuwa kwenye
kibanda hicho , walianza kuhamaki kasha kumtafuta mwenyekkiti wa eneo hilo kwa
lengo la kumkamata muhusika huyo na kumshitaki polisi.
Aidha,
imeelezwa kuwa awali muhusika huyo, alipohojiwa kwamba ni kweli nyama hiyo
ilikuwa ya mbwa, inadaiwa kwamba alikiri lakini hakueleza sababu iliyompelekea kuuza
nyama hiyo.
Hata
hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea
kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa amekamatwa na atafikishwa mahakamani mara
upelelezi utakapo kamilika.
Kamanda
Msangi, amewataja baadhi ya watu waliodaiwa kuuziwa kitoweo hicho ni Enock
Nsemwa(52) mkazi wa Ngyekye na Anyandwile Mbwilo (29) wote wakazi wa kijiji
hicho na kwamba ameihasa jamii kuwa makini hususani wanaponunua vyakula ili
kujiepusha na madhara ya kiafya.
Mwisho.








Post a Comment