Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Askofu Mkuu Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Mbeya Alinikisya Cheyo
 Na  Emanuel Madafa, Mbeya.
KANISA la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi, limesema umefika wakati wa kuwasilisha  mgogoro unaoendelea ndani ya kanisa hilo kwa kamati teule ya usuluhishi wa migogoro ya kanisa nchini inayoongozwa na Askofu Alex Malasusa.

Mgogoro huo ambao hivi karibuni ulisababisha baadhi ya waumini na wachungaji wa dhehebu hilo kuzifunga ofisi za Jimbo huku wakitishia kuchafuka kwa hali ya amani endapohalmashauri kuu ya jimbo haitamrudisha madarakani aliyekuwa Mwenyekiti wa kanisa hilo,Nosigwa Buya baada ya kusimamishwa kwa tuhuma zakushindwa kusimamia matumizi ya fedha, hivyo kuliingizia kanisa hasara ya mamilioni ya fedha.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo , askofu Mkuu wa kanisa hilo, Alinikisya Cheyo, alisema wakati umefika kwa viongozi wakubwa wa kiroho kuingilia kati mgogoro huo na kuumaliza kuliko kuendelea na mabishano ya pande mbili ambayo hayafikii muafaka licha ya serikali kuingilia kati.

Amesema, anatarajia kukutana na kamati hiyo teule ya usuluhishi inayoongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)  Alex Malasusa pamoja na Askofu Mkuu wa kanisa la Anglikana Jaji mstaafu  Agustino Ramadhani kwa ajili ya kuomba ushauri wa nini kifanyike ili kumaliza mgogoro huo.

Alisema, wao kama kanisa wamefika mahala wameshindwa kufikia muafa kutokana na muingiliano wa pande mbili ambazo zimekuwa zikisigana hivyo kulifanya jambo hilo kuendelea kuwa kubwa na gumu.

Amesema, baadhi ya wajumbe walikuwa wakionyesha kukubali yaishe kwa kulimaliza suala hilo kwa kuombana msamaha na kumrudisha Mwenyekiti Buya madarakani lakini wengine walikubali kumsamehe lakini si kurudi madarakani kwa kiongozi huyo.

Hata hivyo, Askofu huyo, amekiri kwamba halmashauri hiyo imefikia muafaka wa kuitisha mkutano mkuu wa Sinodi ifikapo Disemba mwaka huu katika kulitatua tatizo hilo.
Mwisho.


 Askofu Alex Malasusa.

Hali ilivyokuwa wiki moja kabla ya askofu cheyo kutoa tamko Makao makauu ya kanisa hilo Jakaranda jijini Mbeya .



Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top