Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na Mwandishi wetu,Mbeya
Wachezaji 20 wa mpira wa kikapu Mkoa wa Mbeya, wanatarajia kushiriki mashindano ya Taifa CUP, yatakayofanyika  Mkoani Dodoma  November 23 hadi November 30 mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kupokea Katibu wa timu hiyo, Yusuf Nyirenda, alisema kuwa wanawashukuru Coca Cola  kwa kuchangia kiasi hicho cha fedha .
 "Kwa kushirikiana na Coca Cola, tunaamini kuwa mpira wa kikapu utapata msukumo mkubwa na kupiga hatua zaidi nchini lakini bado tunakabiliwa na changamoto ya kifedha,” alisema Nyirenda.

Alisema, timu inatajia kuondoka Mbeya November 20, ikiwa na wachezaji 20 kati yao wanawake 10 na wanaume 10 lakini mpaka sasa  wamefanikiwa kupata shilingi milioni moja kati ya milioni 4,700,000 zinazohitajika.

“Kiasi cha shiringi milioni 4,700,000 kinahitajika kwa ajiri ya usafiri wa kwenda na kurudi, chakula, malazi na ada ya kushiriki mashindano haya,”alisema.

Alisema, gharama hizo ni kwa wachezaji 10 wanaume ,wanawake 10 na viongozi wawili ambao wataondoka na timu hiyo lakini bado timu inauhitaji wa shilingi milioni 3,600,000 hivyo kuwaomba wadau kujitokeza kuichangia timu hiyo ili iweze kushiriki..

Meneja kutoka Kampuni ya vinywaji baridi ya Coca Cola Haji Ally , alisema wanajua kuwa mashindano ya mwaka huu yatashirikisha mikoa mbalimbali  hivyo wametoa  kiasi hicho cha fedha katika kuisaidia timu ya Mbeya kushiriki mashindano hayo.

Hata hivyo, aliwaomba wadau  na mashabiki wa mpira huo, kujitokeza kwa wingi katika kuichangia timu hiyo ili iweze kufika Mkoani Dodoma na kushiriki mashindano hayo.


Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top