Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Milola jimbo la Mchinga ambapo aliwaambia wapinzani wamekosa sera mbadala matokeo yake wamekuwa wakitumia muda mwingi kuishambulia CCM
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Milola, wilaya ya Lindi Vijijini ambapo aliwaambia CCM imejipanga vizuri kuwashinda Upinzani kuanzi Serikali za mitaa
  Mbunge wa Jimbo la Mchinga Ndugu Said Mtanda akihutubia wakazi wa Milola ambapo aliwaambia asilimia kubwa za ahadi zake zimetimia.
  Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM ,Mbunge wa Jimbo la Mtama na mlezi wa wilaya Kilwa na Waziri wa Mambo ya Nje Ndugu Bernard Membe akiwasalimia wakazi wa Milola waliojitokeza kwa wingi kuja kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman.
 Sehemu ya wakazi wa Milola wakifuatilia mkutano
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye pich ya pamoja baada ya kuwakabidhi vyeti vya kuhitimu mafunzo ya kuendesha boda boda.

Kwa Picha zaidi bofya hapa.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top