| Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abas Kandoro |
Na Mwandishi wetu
SERIKALI Mkoani Mbeya, imelazimika kukifunga kiwanda
cha Bale Fruits&Beverages Enterprises kinachozalisha bidhaa aina ya juice
kwa muda usiojulikana kutokana na kukiuka taratibu za uzalishaji.
Bidhaa zinazo tengenezwa na kiwanda hicho bubu zimekuwa z imekuwa zikiuzwa kwa shilingi 300 hadi 400 kwa watumiaji ambao asilimia kubwa ni watoto.
Kiwanda hicho kilichopo katika eneo la Itiji lililopo
Jijini Mbeya, kimekuwa kikizalisha bidhaa hiyo ya juisi maharufu ikiwa na nembo
ya biashara “Halisi Orange Drink” na kuisambaza kwa walaji waliomo ndani
ya Jiji la Mbeya na Mkoa wa jirani wa Ruvuma.
Akizungumzia uamuzi wa kukifunga kiwanda hicho, Mkuu wa
Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro, amesema serikali ilipokea taarija ya uwepo wa
kiwanda hicho na tayari imetoa maelekezo kwa Mamlaka ya Chakula na
Dawa kukifunga haraka iwezekanavyo.
Kandoro, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama
ya Mkoa wa Mbeya, alisema serikali hairuhusu mtu yoyote kuanzisha
kiwanda bila ya kufuata taratibu za kisheria hivyo ni vema kiwanda hicho
kikafungwa ikiwa na kukamatwa kwa mmiliki huyo.
Akizungumzia sakata hilo, Meneja wa Mamlaka ya Chakula na Dawa
Nyanda za Juu Kusini, Rodney Alananga, alikiri kupokea taarifa hiyo
na kuifanyia kazi kwa kukifunga kiwanda hicho na kuthibitisha kwamba bidhaa
hiyo si salama kwa afya ya mlaji kutokana na kutokaguliwa na TBS.
Alisema, November 7, mwaka huu timu ya TFDA ikiongozana na
wataalamu kutoka halmashauri ya Jiji la Mbeya ilifika katika eneo la tukio na
kujionea hali halisi ya mazingira ya kiwanda hicho kwamba si rafiki
hivyo kuamuru kufungwa kwa kiwanda hicho.
Aidha, Alananga alishindwa kuweka bayana hatua
zilizochukuliwa na uongozi huo katika kudhibiti bidhaa ambayo tayari
imeingia sokoni na walaji wameendelea kuitumia.
Hata hivyo, akizungumzia tuhuma hizo mmiliki wa Kiwanda hicho,
Jonas Bushambali, kwa njia ya simu, alisema yeye yupo njiani anaelekea Jijini
Dar es Salaam na kuwataka waandishi wa habari kuonana naye siku ya Jumanne ya
wiki ijayo kwani hawezi kulizungumzia suala hilo kwa njia ya simu.
Akizungumzia madhara yatokanayo na bidhaa hiyo kwa walaji,
Mganga Mkuu wa halmashauri ya Jiji la Mbeya, Samweli Lazalo, alisema walaji
wapo hatarini kukumbwa na homa za matumo kutokana na bidhaa hizo kuzalishwa
chini ya kiwango na katika mazingira machafu.
Mbali, na homa za matumbo, pia Lazalo akiri wazi kwamba kutokana
na bidhaa hiyo kutokaguliwa hivyo kiwango cha kemikali kilichotumiwa
ndani hakijulikani .
![]() |
| Bidhaa inayotengenezwa na kiwanda hicho. |
JAMIIMOJABLOG








Post a Comment