| Bweni linalokaliwa na wanafunzi wa kiume |
| Hapa Ndipo wanapo lala wanafunzi hawa |
| Muda wa chakula ambapo huo ni wamara moja tu kwa siku na mwendo wa kabegi na Nguna yani ugali |
| Hili ndilo bweni la wasichana na ni sehemu ya kulia chakula.soma habari kamili |
NaMwandishi wetu,Mbeya
SERIKALI Wilayani Mbeya, imefikia uamuzi wa kukifunga chuo cha Mchepuo wa Kilimo cha Nice Dream, kilichopo Jijini Mbeya, baada ya uongozi kuwatelekeza wananfunzi wa chuo hicho pamoja na kufanikiwa kuondoka na mamilioni ya fedha yaliyotokana na ada za watoto hao.
SERIKALI Wilayani Mbeya, imefikia uamuzi wa kukifunga chuo cha Mchepuo wa Kilimo cha Nice Dream, kilichopo Jijini Mbeya, baada ya uongozi kuwatelekeza wananfunzi wa chuo hicho pamoja na kufanikiwa kuondoka na mamilioni ya fedha yaliyotokana na ada za watoto hao.
Chuo hicho ambacho kinasemekana hakitambuliwi na serikali
kilianzishwa mwezi September mwaka huu katika mtaa wa Mapelele Kata ya Ilemi
iliyopo ndani ya Jiji la Mbeya kikiwa na wananfunzi 48.
Hata hivyo, imeelezwa kwamba mbali na wananfunzi hao kutapeliwa
fedha zao, pia wamekuwa wakiishi kwa kusaidiwa chakula na majirani
wanaokizunguka chuo hicho.
Akizungumzia sakata hilo, Diwani wa Kata hiyo, Furaha Mwandalima,
alikiri uwepo wa chuo hicho na kudai kuwa yeye alipokea malalamiko kutoka kwa
baadhi ya wanachuo ambapo alifika kwenye eneo la tukio na kujionea hali
halisi.
Aidha, amesema kuwa baada ya kuona hali hiyo, alitoa taarifa kwa
uongozi wa juu ambao walitoa maelekezo yaliyowataka wanafunzi hao
kujihoredhesha majina yao ili serikali iangalie utaratibu wa kuwarudisha makwao
na Chuo kifungwe.
Amesema, kwa mujibu wa taarifa aliyoipata ni kwamba wanafunzi 42
wanatokea Mkoa wa Kagera na wawili wakitokea mkoani Mara ambapo wawili
wanatokea wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya hali mmoja akitokea Mkoa wa Dar es
Salaam.
Mmoja wa wanachuo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema waliletewa taarifa na wakuu wa shule walizokuwa wakisoma baada ya
kumaliza kidato cha nne mwaka uliopita kuwa wamechaguliwa na serikali kusomea
Kilimo Mkoani Mbeya lakini walipofika walishangazwa na hali waliyoikuta na
kwamba walipofuatila kwenye mtandao walibaini chuo kutosajiliwa katika Baraza
la Vyuo.
Walipoutafuta uongozi wa Chuo hicho ulianza kupiga chenga ndipo
walikwenda kutoa taarifa Polisi na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ambapo uongozi wa
Wilaya umeanza hatua za kumtafuta mmiliki ili aweze kutoa majawabu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, alisema askari
wa kitengo cha upelelezi wanafuatilia suala hilo ili kuwatia nguvuni wahusika
na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Hata hivyo, aliwashauri wanafunzi hao kuanza kutafuta njia mbadala
ya kujiendeleza kielimu kwa kutafuta vyuo vingine kuliko kuendelea kupoteza
muda wao wakiendelea kuwasubili wahusika hao ambao mpaka sasa hawajulikani
walipojificha.
Mwisho.






Post a Comment