| Meneja Mkuu wa Pepsi Ndugu Sanjay Monshi akizungumza katika uzinduzi huo ambao umefanyika katika kiwanda cha Pepsi Iyunga jijini Mbeya. |
| Meneja Mauzo Kampuni ya vinywaji baridi vya Pepsi Ndugu Ommary Jumbe akizungumzia lengo la shindano hilo. |
| Afisa Rasilimali watu Kampuni ya Pepsi Ndugu Edwin Arbogast |
Kampuni ya SBC Tanzania Limited Watengenezaji na wasambazaji wa vinywaji baridi aina ya Pepsi,Mirinda,7up,Mountain Dew na Evervess wamezindua shindano maalum linalojulikana kama Jishindie Mamilioni kila siku na Pepsi.
Shindano hilo litahusu Soda aina ya Pepsi ,Mirinda Orange ,Mirinda Fruty,Mirinda Green Apple ,pamoja na MountainDew (300mil) na seven up zenye ujazo wa milimita 350 tu.
Akizungumza katika uzinduzi huo Meneja Mkuu wa Pepsi Ndugu Sanjay Munshi amesema shindano hilo litaendeshwa kuanzia Nov 10 hadi Des 21 mwaka huu ambapo litahusisha mikoa ya Dar es salaam,Pwani,Morogoro,,Dodoma,Mtwara,Iringa,Njombe Ruvuma Rukwa na Katavi.ambapo vizibo vya shindano la jishindie Mamilioni kila siku na Pepsi vitakuwa narangi ya dhahabu .
Amesema shindano hilo litakuwa na zawadi na pesa tasilimu kiasi cha shilingi 2,500,000 na ,1,000,000 pamoja na 500,000 huku zawadi nyingine zikiwa ni soda za bure .
Aidha kwa upande wake Meneja Mauzo wa Pepsi Mbeya Ndugu Omary Jumbe amesema ili mteja ajishindie zawadi anatakiwa kununa soda za jamii yaP epsi kisha abandue ganda ndani ya kizibo ambapo anaweza kukuta maandishi ya viwango hivyo vya feza au zawadi ya Soda na kubahatika kuibuka mshindi.
mwisho.






Post a Comment