Na Mwandishi wetu,
Mbeya.
Watumishi 11 wa Kanisa la Moraviani Tanzania, Jimbo la Kusin Magharibi,wameshindwa kupata malipo yao ya mishahara kwa miezi mitatu baada ya klabu ya timu ya mbeya city kudaiwa kushindwa kulipa deni la shilingi milioni 19.
Deni hilo limetokana na Timu hiyo ya mbeya City kutumia hostel na malazi, wakati wa
maandalizi ya msimu wapili wa ligi kuu ya Vodacom 2013.
Timu hiyo, ambayo iliweza kujizolea mashabiki wengi ukilinganisha na timu kongwe za Yanga na
Simba kwa msimu uliopita, imetajwa kukwamisha baadhi ya shughuli za kanisa hilo
pamoja na wafanyakazi 11 kutolipwa mishahara yao, kutokana na kushindwa kulipa
kiasi hicho cha fedha kwa wakati.
Akizungumza na blog hii Meneja wa Hosteli
Msaidizi, Tuntufye Mwachuga alisema kiasi hicho cha fedha ni malipo ya kipindi
cha miezi miwili walichotumia uongozi wa timu hiyo, kipindi cha msimu wa pili
wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa mwaka 2013.
“Uongozi wa klabu hii ya Mbeya City, walifika ofisini na
kuingia mkataba wa wachezaji wake kuweka kambi kwenye hosteli hii kwa malazi na chakula kilichojumuisha milo
mitatu, asubuhi, mchana na jioni kwa kipindi chote cha miezi miwili watakacho
kitumia na sisi kukubaliana nao,”alisema.
Alisema, baada ya makubaliano hayo timu ilikaa na kumaliza
muda wake huku timu ikifanikiwa kufanya vizuri lakini cha ajabu ni pale,
uongozi wa kanisa ulipoanza kufuatilia malipo
na kuanza kupigwa kalenda kitendo ambacho hatujapendezwa nacho.
“Kanisa linaidai klabu ya Mbeya City kiasi cha shilingi
milioni 19, 681,000 kwa malipo ya malazi na chakula katika kipindi cha miezi
miwili walichotumia wakati walipoweka kambi msimu uliopita wa ligi kuu ya Vodacom tangu February 3 hadi
April 17 mwaka 2014 ,”alisema.
![]() |
| Katibu wa Mbeya City Emanuel Kimbe |
Akizungumzia deni hilo, Katibu wa klabu ya Mbeya City,
Emmanuel Kimbe, alikiri uwepo wa deni na kwamba tayari taratibu za malipo
zinaendelea.
“Kila Taasisi inayojiendesha hudai na kudaiwa, kwa hiyo Mbeya
City kama Taasisi inayojiendesha inadaiwa pia lakini tunaendelea na mchakato wa
malipo,”alisema Kimbe.
Alisema, malipo hayo yameanza kufanyika tangu Alhamis na
ijumaa ya wiki iliyopita hivyo aliwaomba wadai kuwa wavumilivu.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Mussa Zungiza, akitolea
ufafanuzi suala hilo, alisema halmashauri haihusiki na deni hilo kwani timu
ya Mbeya City inauongozi wake na
inajiendesha yenyewe kwa kila kitu.
Mwisho.







Post a Comment