Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na Mwandishi wetu Mbeya
JESHI la Polisi Mkoani Mbeya, linawashikilia madereva watatu wa mabasi ya abiria yanayofanya safari zake kati ya Mbeya na Dar es salaam, baada ya kukutwa wakijiandaa kusafirisha abiria wakiwa wamelewa.

Katika sakata hilo, mabasi mengine matatu pia yametozwa faini na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) kwa kosa la kutokuwa na madereva wawili pamoja na vibali vya kusafirisha abiria.

Watuhumiwa hao walikamatwa jana wakati Jeshi hilo na Sumatra walipofanya ukaguzi wa kushtukiza kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi cha Jijini Mbeya.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya, Butusyo Mbwambelo alisema kuwa madereva hao wamekamatwa baada ya kupimwa na kukutwa na viwango mbalimbali vya ulevi.

Alisema Madareva wawili kati yao ni wa Kampuni ya Nganga na dereva mmoja ni wa kampuni ya Alhushoom ambayo yanafanya safari zake kati ya Mbeya na Dar es Salaam.

Amesema, kwa kawaida dereva hapaswi kuzidisha kiwango cha ulevi cha mg 0.8, lakini madereva hao walikuwa na kiwango cha juu cha ulevi cha mg 13.0,  118.0 na mg 123.0.

Amesema kuwa dereva mwingine baada ya kupimwa na kubainika kuwa amelewa alikimbia na hivyo Jeshi la Polisi linaendelea kumtafuta ili sheria iweze kuchukua mkondo wake na kwamba madereva waliokamatwa watafikishwa mahakamani.

Kwa upande wake Afisa Mfawidhi Sumatra mkoani Mbeya, Denis David amebainisha kuwa  katika ukaguzi wake, alibaini kuwepo kwa mabasi matatu yanayosafiri umbali mrefu ambayo hayakuwa na madereva wawili kama ambavyo masharti ya leseni yanavyoelekeza.

Amesema kuwa mabasi hayo yametozwa faini ya shilingi 250,000 kila moja na kutakiwa kutafuta dereva wa pili kabla ya kuanza safari.
Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top