![]() |
| Waziri wa Maliasili na Utalii Razalo Nyarandu, |
Na Mwandishi wetu,Mbeya
SERIKALI Nchini, imeamua kuachana na maeneo ya ardhi ya wananchi
wa Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya, ambayo yalipendekezwa kuingizwa kwenye
hifadhi ya Taifa ya Tanapa.
Maeneo hayo ya wananchi yenye ukubwa wa kilomita za mraba 10,000 yamedaiwa
kuidhinishwa na kamati ya ushauri ya mkoa wa Mbeya (RCC) kwa ajili ya kuingizwa
kwenye hifadhi ya Tanapa jambo lililosababisha kuibuka kwa migogoro baina
wananchi na Tanapa.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Mbeya jana, Waziri wa Maliasili na
Utalii Razalo Nyarandu, alisema serikali imeamua kuachana na maeneo hayo ya
wananchi ambayo yalipendekezwa na uongozi wa Mkoa wa Mbeya kuingizwa
kwenye hifadhi ya Tanapa.
Alisema, moja ya taratibu ambazo Mkoa unapaswa kuzifuata ni pamoja
na kutenga fedha za fidia za kuwalipa wahanga hao pamoja na kuwaandalia maeneo
husika ambayo miundombinu yake itakuwa imekamilika.
Naye Mbunge wa Jimbo la Mbarali, Modestus Kirufi, alitumia nafasi
hiyo kuishukuru serikali kwani uamuzi huo umesaidia kupunguza idadi ya migogoro
ya ardhi ambayo imekuwa ikishamiri katika eneo hilo la Wilaya ya Mbarali.
mwisho.







Post a Comment