Na Emanuel Madafa,Mbeya
Mtu mmoja mwenye asili ya Kisomali na Kiethiopia ambaye hakuweza
kufahamika jina, jinsi ya kiume, mwenye umri kati ya miaka 25-30 amekutwa
amekufa vichakani mita tatu kutoka barabara kuu ya mbeya/tunduma
Mwili wa marehemu ulikutwa eneo la Kijiji cha Kilimampimbini, Kata ya Vwawa,
wilaya ya mbozi, mkoa wa mbeya mnamo Desemba
10 mwaka huu majira ya saa 15:00 alasiri.
Aidha Mwili wa marehemu huyo umekutwa ukiwa hauna jeraha lolote na ukiwa
umedhoofika sana.
Aidha baada ya kupekua mfukoni alikutwa na tiketi ya basi la Ratco
express iliyokuwa na jina la ely family mdundo kutoka Tanga kwenda dsm
iliyokatwa Novemba 04 mwaka huu ambayo
ilitakiwa kutumika Nov 6 mwaka huu
Kwa mujibu wa taarifa kutoka jeshi la Polisi Mkoani humo Inadhaniwa kuwa
marehemu alikuwa ni mhamiaji haramu.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya serikali wilaya ya mbozi.
Uchunguzi zaidi wa tukio hili unaendelea.
Hata
hivyo katika hatua nyingine Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linawashikilia raia wanne wa nchini kongo kwa
kosa la kuingia nchini bila kibali.
Wahamiaji hao ni pamoja na Hassan Kaula (18) Katumba Asheri (20) Issah lukimbana (20) na Ibele Buma (20).
Watuhumiwa walikamatwa mnamo tarehe 10.12.2014 majira ya saa 13:20
mchana katika msako uliofanyika huko katika eneo la kasumulu mpakani, Kata ya Ngana
Wilaya ya Kyela, Mkoa wa mbeya huku Taratibu za kuwakabidhi idara ya uhamiaji kwa
hatua zaidi za kisheria zinaendelea.







Post a Comment