Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkuu wa Mkoa wa mbeya Abbas Kandoro (katikati) akiwa pamoja na viongozi na wakuu wa wilaya ya mkoani humo katika mkutano na waandishi wa habari juu ya ukamilishwa wa zoezi la ujenzi wa maabara.
 Na Emanuel Madafa, Mbeya.
SERIKALI ya Mkoa wa Mbeya, imeweza kutekeleza agizo la Rais  Jakaya  Kikwete la ujenzi wa maabara kwa asilimia 95.45 kwa shule 696 zilizopo mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo  jijini Mbeya , Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro, amesema Mkoa wa Mbeya unajumla ya shule za sekondari 696 zinazomilikiwa na serikali na kati ya hizo shule 602 zimekamilisha ujenzi wa vyumba hivyo vya maabara.

 Kandoro amezitaja halmashauri ambazo tayari zimekamilisha zoezi hilo kuwa ni Halmashauri ya Mbeya, ambayo inajumla ya shule 27 za sekondari na maabara zilizokuwa zikihitajika ni 81 na zote zimekamilika  sambamba na vitendea kazi vyake.

Amesema, halmashauri nyingine ni Kyela ambayo inajumla ya sekondari 22 uhitaji wa maabara ulikuwa ni 66 na zote zimekamilika ikifuatiwa na halmashauri ya Mbozi ambayo inajumla ya sekondari 40 maabara zilizokamilika ni 117 kati ya 120 zinazohitajika.

Amesema, ujenzi wa vyumba hivyo vya maabara umeenda sambamba na tarehe ya mwisho aliyoitoa Rais ya kwamba ifikapo mwezi  Desember  mwaka huu, halmashauri zote nchini ziwe zimekamilisha ujenzi  huo wa maabara.

Amesema, vyumba vya maabara  94 sawa na asilimia 4.55 ujenzi wake bado unaendelea lakini  ifikapo mwezi Desember mwaka huu vitakuwa vimekamilika kwani matengenezo yaliyobakia ni madogo madogo.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amesema  halmashauri ya Mbarali ambayo  imekamilisha ujenzi huo wa maabara 48 kati ya 48 zilizokokuwa zikihitajika huku  halmashauri ya  Busokelo ambayo inajumla ya shule 15 maabara zilizokamilika ni 41 kati ya 45 zinazohitajika , halmashauri ya Chunya shule zilizopo 20 maabara  60 zilizokamilika ni 18.

Hata hivyo, Kandoro amesema kuwa halmashauri ya Ileje inajumla ya shule 19 na maabara zilizokamilika 51 kati ya 56 zinazohitajika huku Jiji la Mbeya  likiwa na shule 31 maabara zinazohitajika ni 93 kati ya hizo maabara 89 zimekamilika.
Mwisho.





Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top