Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka akizungumza na waandishi wa habari kwenye hotel ya Hyatt Regency Dar Es Salaam, The Kilimanjaro  
.
Dar es Salaam,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Profesa Anna Tibaijuka,amekutana na waandishi wa habari na kuzungumzia sakata la Akaunti ya Escrow,huku akisema haoni sababu ya yeye kujiuzulu kutokana na kudaiwa kuhusika katika sakata hilo.

 Alisema hawezi kufikia uamuzi wa kujiuzulu kwa kuwa hana kosa kwani hajatajwa mahala popote katika ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali ( CAG ),ingawa hakupewa nafasi ya kujitetea na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alisisitiza fedha alizopewa na Rugemalila ni mchango wa Shule ambapo alisema lengo lake kuwasaidia watoto wa kike kupata elimu bora.
 Alipoulizwa kuhusu kujiuzulu  alisema hawezi jiuzulu kwani haoni sababu ya yeye kujiuzulu.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top