Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya Ndugu Veronica Kessy


Na Emanuel Madafa,Mbeya

MAHAKAMA Kuu (MBEYA), inatarajia kuwafungulia kesi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rungwe Veronica Kessy na Mkurugenzi wa Kampuni ya Mek One Mohamed Awadh , baada ya kukiuka agizo la mahakama lililowataka kutofanya jambo lolote  katika kituo cha mafuta cha Gapco mpaka kesi ya msingi namba 6/2013 iliyopo kwenye mahakama ya Wilaya itakapotolewa maamuzi.



Agizo hilo lilitolewa  na Mahakama kuu Oktoba 8, 2013 na Jaji Atuganile Ngwala, baada ya Halmashauri ya Rungwe ambayo inamiliki kituo hicho cha mafuta kudaiwa kuingia mkataba na Kampuni ya mafuta ya Mek One , wakati mkataba wa awali walioufanya na kampuni ya mafuta ya GAPCO haujamalizika muda wake, kinyume cha sheria namba 114(i) (k) sura ya 16 ya mwaka 2002.



Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Msajili wa Mahakama, Aron Lyamuya, alisema kutokana na wahusika hao kukiuka agizo hilo lililotolewa na Jaji Ngwala, Mahakama hiyo inatarajia kuwafungulia kesi watuhumiwa hao.





 Amesema, Mahakama hiyo ilipokea  maombi kutoka kwa  Kampuni ya mafuta ya GAPCO  yenye namba 76/2014 ambayo  ilieleza kwamba  mmiliki huyo,halmashauri ya Rungwe kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa kampuni ya Mek One, wameingia mkataba na kuanza kuendesha shughuli ya uuzaji wa mafuta  licha ya mahakama hiyo kuzuia.



Amesema, kutokana na agizo hilo, mahakama inatarajia kuzungumza na Mwanasheria wa serikali na ofisi ya upelelezi Mkoa wa Mbeya(RCO) ili kuona utaratibu wa kuwafungulia mashitaka wawatuhumiwa wote wawili kutokana na kukaidi agizo hilo la Mahakama.


Mwisho.



Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top