Wakazi wa Mtaa wa Ilemi juhudi jijini Mbeya wakiwa tayari kukabidhiwa msaada huo. |
Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya Quip Mbeyela akizungumza katika makabidhiano ya Msaada huo. |
Kaimu Mkurugenzi jiji la Mbeya Dkt Samwel Lazaro akizungumza kabla ya kukabidhi msaada huo kwa waathirika wa janga hilo.Picha na David Nyembe Fahari News |
Na Emanuel
Madafa,Mbeya
Halmashauri ya jiji la Mbeya imetoa msaada kwa Wananchi wa Mtaa
wa Ilemi jijini Mbeya kufuatia makazi
yao kuharibiwa vibaya na mvua iliyoambatana na upepo mkali hivi karibuni na kusababisha athari kubwa kwa
wananchi hao .
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada
huo Kaimu Mkurugenzi Halmshauri ya jiji la Mbeya Dkt Samwel Lazaro amesema
baada ya kupata taarifa za janga hilo uongozi wa halmashauri hiyo ulikaa na
kujadiliana namna ya kutoa msaada kwa waathirika hao.
Amesema katika majadiliano hayo
uongozi huo ulikubaliana na kuamua
kutoa mchango wao ambao Sukari kilo 3 kwa kila kaya pamoja na Unga wa ugali
mfuko mmoja wa kilo 10 na Maharagwe kilo 1.
Amesema pamoja na kutoa msaada huo
lakini pia uongozi wa halmshauri hiyo umeanza mchakato wa kufanya tathimini
ili
kutambua hali halisi ya uhalibifu huo.
|
Aidha Dkt
Lazoro amesema kuwa kutokana na baadhi ya miundo mbinu ya shule ya Msingi Ilemi
kuharibiwa kwa kuezuliwa mapaa yake pamoja na vyoo tayari mafundi wamekwisha anza
utaratibu wa kufanya ukarabati kwa gharama za serikali pasipo kuwa husisha
wananchi .
Mvua hizo
zilizo nyesha hivi karibuni jijini hapa zilileta madhara hayo kwa kuharibu
baadhi ya miundo mbinu ya shule ya msingi Ilemi pamoja na kuharibu makazi ya
watu kwa kaya zaidi ya 38 na kupelekea wakazi hao kukosa mahali pa kuishi
pamoja na kuhitaji msaada wa maradhi mbalimbali.
Mwisho.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.