![]() |
| Kazi ya ushushaji mabango ikiendelea |
Na Mwandishi wetu
KAMPUNI ya Jagro Limitted,
leo imeshusha mabango ya matangazo yanayomilikiwa na Kampuni ya Continental
yenye makao makuu yake Jijini Dar es Salaam, baada ya kushindwa kulipa ushuru
wa zaidi ya milioni 100 kwa halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Kiasi hicho cha fedha ni
malipo ya ushuru katika mwaka wa fedha wa 2014 na 2015, ambapo Kampuni hiyo ya
Continental ikiwa na dhamana ya kutangaza matangazo ya biashara kutoka kwenye
mashirika na makampuni mbalimbali kwa
kutumia nguzo za mabango ya chuma.
Akizungumza na waandishi wa
habari, leo katika eneo la tukio la stendi kuu ambapo zoezi hilo lilikuwa
likifanyika, Mkurugenzi wa Kampuni ya Jagro, Maulid Khamis, anasema kampuni hiyo inatekeleza agizo la halmashauri
ya Jiji laMbeya linalowataka kuyashusha mabango ya matangazo ya biashara
kutokana na wahusika kushindwa kulipa kodi kama sheria ndogo za halmashauri
zinavyowataka.
Amesema, kwa mujibu wa
sheria ndogo ya halmashauri ya Jiji la Mbeya ya mwaka 2014 na sheria ya fedha
ya serikali za mitaa ya mwaka 2012 inayowataka wamilikki wa matangazo kulipia
matangazo hayo kwa kuzingatia sheria ndogo zinazopitishwa na halmashauri
husika.
Anasema, kutokana na sheria
hizo kukiukwa, halmashauri imetoa kibali kwa kampuni ya Jagro kuyashusha
mabango hayo ikiwa ni moja ya majukumu waliyoingia mkataba na halmashauri hiyo
ya Jiji la Mbeya.
Akizungumzia
hilo,Mwanasheria wa Kampuni hiyo ya Jagro, Aloyce Mrema, anasema mbali na
mabango hayo kushushwa pia wamiliki watafikishwa mahakamani .
Mwisho.














Post a Comment