![]() |
| Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi. |
Na Emanuel Madafa,Mbeya
Vitendo vya kikatili na unyanyasaji wa
wanawake na watoto vimeendelea kushika kasi licha serikali na mashirika
mbalimbali na haki za binadamu kupiga
vita vitendo hivyo kwa nguvu vimeendelea kujitokeza tena mkoani hapa.
Hali imejitokeza katika kijiji cha Iwezi Mbozi
pamoja na Ilolo jijini Mbeya.
Katika tukio la kwanza Mkazi wa Mtaa wa Ilolo
jijini Mbeya Ndugu Gwandumbi Kipenya (32) amemuua Mke wake kwa kumpiga nondo
kichwani Ndugu Zainabu Gwandumbi [29] kisha
na yeye kujiua kwa kujinyonga .
Tukio
hilo lilitokea Feb 08 mwaka huu majira
ya saa 09:00 usiku katika mtaa wa ilolo,kata ya sinde, jijini mbeya ambapo inadaiwa kuwa . Mara baada ya kufanya mauaji hayo
mtuhumiwa Gwandumbi kipenya aliingia chumbani na kujinyonga kwa kutumia mkanda
wa begi hadi kufa.
Hata hivyo Chanzo cha matukio hayo bado kufahamika kwani hakuna ujumbe wowote
uliokutwa ndani ya nyumba hiyo.
Wakati huo huo jeshi la Polisi Mkoani Mbeya
linamshikilia Mkazi wa kijiji cha Iwezi Wilayani Mbozi Mkoani Mbeya Ndugu
Saidia Laison Mbagwa [65], baada ya kumfungia ndani
ya nyumba mtoto wake ambaye ni mlemavu.
Tukio hilo lilitokea Feb 08 mwaka majira ya saa 16:00 jioni katika kijiji cha iwezi,kata ya igamba Wilayani
Mbozi.
Katika
tukio hilo mhanga ambaye ana matatizo ya akili na kuanguka ugonjwa wa kifafa,
alikutwa amefungwa kamba miguuni na kunyanyapaliwa kwa kufungiwa chumba maalum
kwa muda wa miezi miwili hivyo
kupelekea kudhoofu afya na kupelekwa
hospitali ya serikali wilaya ya mbozi kwa matibabu.
Mtuhumiwa baba mzazi wa mhanga amekamatwa na
taratibu zinafanywa ili afikishwe mahakamani.
Aidha kamanda msangi anatoa wito kwa jamii
hususani wanandoa kutatua matatizo/kero/migogoro yao kwa njia ya
mazungumzo badala ya kujichukulia sheria mkononi kwani inaleta madhara makubwa
kwa jamii na hususani familia.
MWISHO.







Post a Comment